Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Zefania 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Zefania 2:3
44 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Daudi akawajibu: “Ni kweli mutoto alipokuwa muzima, nilifunga na kulia. Nilifanya hivyo maana nilifikiri: ‘Nani anajua? Labda Yawe atanihurumia kusudi mutoto aishi’.


Mumutafute Yawe mwenye nguvu; mumutafute Yawe siku zote.


Maana Yawe anapendezwa na watu wake; yeye anawaheshimisha wanyenyekevu kwa kuwapa ushindi.


Kwa sababu yako ninakusifu katika kusanyiko kubwa la watu; nitatimiza ahadi zangu mbele ya wanaomwabudu.


Kweli, mazuri yako ni mengi sana, unayowawekea wale wanaokuabudu! Unawatendea mazuri mbele ya watu wote wale wanaokukimbilia.


Ujifungie upanga wako, ewe shujaa! Wewe ni mutukufu na mwenye mamlaka.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo “Usiharibu.” Mashairi ya Daudi alipomuponyoka Saulo na kujificha katika pango.


Ulijulisha hukumu yako toka mbinguni. Dunia iliogopa na kunyamaza,


Ukikaa chini ya ulinzi wa Mungu Mukubwa, ukiishi chini ya kivuli cha Mungu Mwenye Nguvu,


ninyi mutawajibu: ‘Hii ni sadaka ya Pasaka kwa Yawe, kwa sababu alipita nyumba za Waisraeli katika inchi ya Misri. Aliwaua Wamisri, lakini sisi hakutuua.’ ” Waisraeli wakainamisha vichwa na kumwabudu Yawe.


Jina la Yawe ni munara imara; mwenye haki anaukimbilia na kuwa salama.


mujifunze kutenda mema. Mufuate sheria ya Mungu, mumusaidie mwenye kuteswa, mumupatie yatima haki yake, mutetee haki za wajane.


Atawaamulia wamasikini kwa haki na kutetea haki za wakosefu katika inchi. Kwa neno lake dunia itaazibiwa, kwa pumzi yake waovu watauawa.


Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


Maana, kweli nitakuokoa na hautauawa kwa vita; utapata faida ya kuokoa maisha yako kwa sababu umeniamini mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wewe unajitakia wewe mwenyewe mambo makubwamakubwa? Usiyatafute! Achana nayo, maana ninaleta maangamizi juu ya wanadamu wote. Pato lako ni hili: nitayaokoa maisha yako kila nafasi utakapokwenda. –Ni ujumbe wa Yawe.


Hawakwenda kulinda sehemu zile za kuta zilizobomoka wala hawajengi kuta mupya kusudi Waisraeli waweze kujilinda wakati wa vita siku ile ambayo mimi Yawe nimeiweka.


Mupande haki kwa faida yenu, nanyi mutavuna wema; mulime mashamba yaliyoachwa, maana wakati wa kutafuta Yawe umefika kusudi awanyeshee haki kama mvua.


Kiburi cha Waisraeli kinawashuhudia wao wenyewe, hawanirudilii mimi Yawe, Mungu wao; wala hawanitafuti kwa ajili ya matukio hayo yote.


Labda Mungu atabadilisha nia yake, na kuacha kutukasirikia, nasi hatutaangamizwa!


Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku za mafungo ya kula chakula ya mwezi wa ine, mwezi wa tano, mwezi wa saba na mwezi wa kumi, zitakuwa nyakati za furaha na shangwe; zitakuwa sikukuu za shangwe kwa watu wa Yuda. Basi, mupende ukweli na amani.


Heri wale wanaokuwa wapole, maana watarizi dunia!


Kwa mwisho, wandugu, sisi tumewafundisha namna gani munavyopaswa kuishi kusudi mupate kumupendeza Mungu. Na kweli, ni vile munavyoishi. Na sasa, tunawaomba na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu, muendelee mbele vizuri zaidi katika mwenendo ule.


Ni vile mulivyojionyesha mbele ya wandugu wote wa kanisa la Makedonia. Na sasa tunawasihi ninyi wandugu, muendelee mbele vizuri zaidi katika jambo lile.


Ninyi mumekwisha kutakaswa kwa njia ya kutii neno la kweli kwa kuwapenda wandugu zenu pasipo unafiki. Basi mupendane kabisa, kwa moyo wenu wote.


Lakini mapambo yenu yanapaswa kuwa ya ndani ya moyo yasiyoweza kuharibika. Sherti mapambo yale yakuwe yenye kutokana na roho ya amani na upole inayohesabiwa kuwa ya bei kali mbele ya Mungu.


Lakini muzidi kukomaa katika neema na katika kumujua Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. Asifiwe, sasa na hata milele! Amina.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ