Yawe akasema: Mutumishi wangu Isaya amekuwa akitembea uchi na bila viatu kwa muda wa miaka mitatu sasa, kama kitambulisho juu ya inchi za Misri na Kushi.
Maana mimi ni Yawe, Mungu wenu, Mungu Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu. Ninaitoa inchi ya Misri kwa ajili ya ukombozi wenu, ninaitoa Kushi na Seba kusudi muachwe huru.
Nitaitia mikono ya mufalme wa Babeli nguvu na kutia upanga wangu katika mukono wake. Lakini nitaivunja mikono ya Mufalme wa Misri, naye atalalamika mbele ya mufalme wa Babeli kama mutu aliyeumizwa vibaya sana.