Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Zefania 2:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Hayo yatakuwa malipo ya kiburi chao, kwa sababu waliwachekelea na kujivuna mbele ya watu wa Yawe wa majeshi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Zefania 2:10
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu hakumuruhusu mutu yeyote awatese; kwa ajili yao aliwaonya wafalme:


Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: ‘Mpaka wakati gani utakataa kujinyenyekeza mbele yangu? Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Lakini ungali unaonyesha kiburi juu ya watu wangu, wala hauwaachi waondoke.


Watu wa Yuda wanasema hivi: Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu, tunajua jinsi alivyojivuna sana; tumesikia juu ya majivuno, kiburi na mazarau yake; lakini majivuno yake hayo ni bure.


Yawe anasema hivi juu ya jirani wabaya za watu wake: Wamegusa sehemu ya urizi wangu, niliowapatia watu wangu Waisraeli! Basi nitawaongoa kutoka katika inchi yao, na hata watu wa Yuda nitawaongoa katika inchi yao.


Namna gani munaweza kusema: Sisi ni mashujaa, na watu wenye nguvu nyingi za vita?


Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu; Moabu ana majivuno sana. Tumesikia juu ya kujiona, kiburi na majivuno yake; tumesikia jinsi anavyojisifu ndani ya moyo.


Uchafu wake ulionekana waziwazi, lakini muji wenyewe haukujali mwisho wake. Anguko lake lilikuwa kubwa sana; hakuna anayeweza kuufariji. Unasema: Angalia, ee Yawe, mateso yangu, maana adui yangu ameshinda.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa sababu mulipiga mikono, mukarukaruka kwa furaha na kushangilia sana juu ya inchi ya Waisraeli,


Siku ile mulisimama pembeni mukiangalia tu, wakati wageni walipouteka utajiri wao, walipoingia katika milango yake na kugawanya utajiri wa Yerusalema kwa kupiga kura. Nanyi vilevile mulikuwa kama wamoja wao.


Kiburi chako kimekudanganya: wewe unayekaa ndani ya mashimo chini ya mawe makubwa na makao yako yapo juu kwenye milima, hivyo unajisemesha: Nani anayeweza kunishusha chini?


Nimeyasikia matusi ya Wamoabu na mazarau ya Waamoni, jinsi walivyowatusi watu wangu na kujivuna kwamba wamenyanganya inchi yao.


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ