Watawala walionitangulia walikuwa muzigo muzito kwa watu wakiwadai chakula na divai. Zaidi ya hiyo waliwalipisha vikoroti makumi ine vya feza. Hata watumishi wao waliwatesa watu. Lakini, mimi sikufanya hivyo, maana nilimwogopa Mungu.
Halafu wabwana wa yule mujakazi wakaona kwamba hawataweza tena kupata mali kutoka kwa yule aliyekuwa kitumaini chao. Kwa hiyo wakakamata Paulo na Sila, wakawakokota na kuwapeleka mbele ya wakubwa kwenye nafasi ya makutano.
Bwana wa mwanamuke yule alipoamuka asubui, akafungua milango ya nyumba, akatoka inje kusudi aendelee na safari. Kwa rafla akamukuta habara yake amelala chini mbele ya mulango, mikono yake ikishika kizingiti cha mulango.
Ndiyo maana makuhani wa Dagoni na wote wanaoingia kumwabudu Dagoni kule Asidodi, wanapoingia kwenye hekalu la Dagoni hawakanyagi kizingiti cha hekalu la Dagoni mpaka leo.