Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Zefania 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Nitawaangamiza wote wanaoinama juu ya dari, wakiabudu jeshi la mbinguni. Nitawaangamiza wale wanaoniabudu na kuapa kwa jina langu, tena wanaapa vilevile kwa jina la mungu Milkomu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Zefania 1:5
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitafanya hivyo kwa sababu Solomono ameniacha, akaabudu miungu ya kigeni: Astaroti mungu wa Wasidoni, Kemosi mungu wa Wamoabu, na Milkomu mungu wa Waamoni. Solomono ameniasi, ametenda maovu mbele yangu. Hakutii masharti yangu na maagizo yangu kama Daudi baba yake alivyofanya.


Solomono alimutumikia Astaroti aliyekuwa mungu wa Wasidoni, na alimufuata Milkomu, mungu wa chukizo wa Waamoni.


Kisha, Elia akawakaribia watu hao, akawaambia: “Mutaendelea kusitasita ndani ya mioyo mpaka wakati gani? Ikiwa Yawe ni Mungu, mumufuate; lakini ikiwa Bali ni Mungu, basi, mumufuate.” Lakini watu hawakumujibu neno lolote.


Watu hawa vilevile walimwabudu Yawe. Walichagua kutoka kati yao watu wa kila aina na kuwafanya makuhani kutumika katika nafasi zenye kuinuka juu na kutoa sadaka kule kwa ajili yao.


Hivi wakamwabudu Yawe, lakini wakati uleule wakiwaabudu vilevile miungu yao waliyoleta kutoka inchi zao.


Basi mataifa haya yalimwabudu Yawe, lakini vilevile walitumikia sanamu zao za madini yenye kuyeyushwa; na mpaka sasa hivi, wazao wao wanaendelea kutenda hivyo kama vile babu zao walivyotenda.


Mazabahu ambayo wafalme wa Yuda walijenga juu ya paa kwenye chumba cha juu cha Ahazi, pamoja na mazabahu ambayo Manase alijenga katika viwanja viwili vya nyumba ya Yawe, aliyabomoa na kuyapondaponda, kisha alitupa mavumbi yake katika kijito cha Kidroni.


Ujumbe wa Mungu juu ya Bonde la Maono. Kuna nini, ee Yerusalema? Mbona watu wote mumepanda juu ya nyumba?


Mumoja atasema: “Mimi ni wa Yawe”, mwingine atajiita kwa jina la Yakobo, mwingine ataandika juu ya mukono wake: “Wa Yawe”, na kujitambulisha kwa jina la Israeli.


Mimi nimeapa kwa nafsi yangu, ninachosema ni ukweli, neno langu halitarudi nyuma: kila mwanadamu atanipigia magoti, kila mutu atafanya kiapo.


Musikilize, enyi watu wa Yakobo, enyi munaojulikana kwa jina la Israeli, ninyi munaokuwa wa uzao wa Yuda. Ninyi munaapa kwa jina la Yawe, na kudai kwamba munamwabudu Mungu wa Israeli; lakini hayo si ukweli wala sawa.


Na kama watajifunza mwenendo wa watu wangu kwa moyo wote, wakiapa kwa jina langu, wakisema “Kama vile Yawe anavyoishi”, kama vile walivyowafundisha watu wangu kuapa kwa jina la mungu Bali, basi watastawi katikati ya watu wangu.


Nyumba za Yerusalema na nyumba za wafalme wa Yuda, ndizo nyumba zote ambazo juu ya paa zao watu walifukiza ubani kwa kutambikia makundi ya nyota, na kuitolea miungu mingine sadaka za divai, zote zitageuzwa kuwa chafu kama Tofeti.


Wakaldea wanaoushambulia muji huu wataingia na kuuteketeza kwa moto; watauteketeza pamoja na nyumba ambazo juu ya paa zake ubani ulifukiziwa kwa mungu Bali na sadaka za divai zilitolewa kwa miungu mingine, kwa kunichokoza.


ukiapa kwa ukweli, kwa kufuatana na sheria, na kwa haki, kwa kusema “Kama vile Yawe anavyoishi”, halafu mataifa yatapata baraka kutoka kwangu, na kutukuzwa kwa sababu yangu.


Juu ya Waamoni, Yawe anasema hivi: Israeli hana watoto? Hana warizi? Mbona basi mungu Milkomu ametwaa Gadi na watu wake wanafanya makao yao katika miji yake?


Ingawa watu wake wanaapa kwa nafsi ya Yawe, viapo vyao ni vya uongo.


Yawe anauliza: Namna gani nitaweza kukusamehe, ee Yerusalema? Watu wako wameniasi; wameapa kwa majina ya miungu ya uongo. Nilipowashibisha kwa chakula, wao walifanya uzinzi, wakakusanyika kwa uwingi katika nyumba za makahaba.


Kisha, mutakuja na kusimama mbele yangu katika hekalu hili linalojulikana kwa jina langu na kusema “Tuko salama”, ingawa munaendelea kufanya mambo hayo yanayonichukiza.


Munaiba, munaua, munafanya uzinzi, munaapa kwa uongo, munamufukizia mungu Bali ubani na kuabudu miungu mingine ambayo hamujapata kuijua.


Itaachwa imetandazwa mbele ya jua na mwezi na nyota zote za mbingu, vitu ambavyo walivyopenda na kuvitumikia, na kuviendea kwa kuuliza shauri na kuviabudu. Mifupa hiyo haitakusanywa wala kuzikwa, lakini itabaki kama vile mboleo juu ya udongo.


Mioyo yao imejaa udanganyifu. Sasa ni lazima wabebe makosa yao. Yawe atabomoa mazabahu zao na kuziharibu nguzo zao.


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


Mulibeba kama vile sasa sanamu za mungu wenu Sakuti mufalme wenu na sanamu za Kiuni mungu wenu wa nyota, vitu ambavyo mulijitengenezea wenyewe?


“Hakuna mutu anayeweza kuwatumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.


Kesho yake karibu na saa sita ya muchana, hao watu watatu wakafika karibu na Yopa, saa ile Petro akapanda juu ya paa kwa kuomba.


Kwa maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Bwana anasema: Kama vile ninavyoishi, kila mutu atapiga magoti mbele yangu, na kila mutu ataitikia kwamba mimi ni Mungu.”


Mumwogope Yawe, Mungu wenu, mumutumikie, muambatane naye na kuapa kwa jina lake.


Mufanye angalisho kusudi wakati mutakapoangalia na kuona nyota, vitu vyote vya mbinguni, musivutwe kuviabudu na kuvitumikia. Vitu hivyo Yawe amewaachia watu wengine waviabudu.


Musishirikiane na mataifa haya yaliyobaki kati yenu. Musiitaje miungu yao wala musiape kwa majina ya miungu yao; musiitumikie wala kuinama mbele yao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ