Zefania 1:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
13 Utajiri wao utanyanganywa, na nyumba zao zitaachwa tupu! Watajijengea nyumba, lakini hawataishi humo. Watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.
Mimi nikauliza: Bwana, mpaka wakati gani? Naye akanijibu: Mpaka wakati miji itakapobaki tupu bila wakaaji, nyumba bila watu, na inchi itakapoharibiwa kabisa.
Yawe anasema: Nitazifanya mali zenu na akiba zenu zitekwe tena, wala hamutapewa malipo yoyote ya vitu hivyo kwa sababu ya zambi zenu zote mulizozitenda kila pahali katika inchi.
Kama simba anavyotoka kwenye maficho yake, mwangamizaji wa mataifa ameanza kuja, anakuja kutoka pahali pake, kusudi aharibu inchi yenu. Miji yenu itabaki mabomoko matupu, bila kukaliwa na mutu yeyote.
Watakula mazao yenu na chakula chenu; watawaua wana na wabinti zenu. Watachinja makundi yenu ya kondoo na ngombe; wataiharibu mizabibu yenu na miti yenu ya matunda ya tini. Miji yenu yenye kuzungukwa na kuta munayoitegemea, wataiharibu kwa silaha zao.
Nami nikauliza: Kuna mutu anayekuwa na hekima apate kueleza mambo haya? Ni nani aliyeongea na Yawe hata aweze kutangaza kwa nini inchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mutu anayepita humo?
Enyi wanawake, musikilize neno la Yawe! Mutege masikio musikie jambo analosema. Muwafundishe wabinti zenu kuomboleza, na kila mutu amufundishe jirani yake wimbo huu wa maziko:
Watatupa feza yao ndani ya barabara na zahabu yao itakuwa kama kitu kichafu. Feza na zahabu zao hazitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe; wala hawataweza kushiba au kujaza tumbo zao feza na zahabu waliyojilundikia; maana mali hiyo ndiyo iliyosababisha zambi yao.
Ninyi munawagandamiza wazaifu na kuwalipisha kodi ya ngano. Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa, lakini ninyi hamutaishi humo; munalima bustani nzuri za mizabibu, lakini hamutakunywa divai yake.