Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Zefania 1:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Mulie, enyi wakaaji wa Makitesi! Wachuuzi wote wameangamia, wote wanaopima feza wameteketezwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Zefania 1:11
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata akilundika feza kama vile mavumbi, na nguo kama vile udongo wa mufinyanzi,


yeye alundike tu, lakini mwenye haki ndiye atakayezivaa, na feza yake watu wasiokuwa na kosa wataigawanyana.


Muomboleze, enyi wachungaji; mulie na kugaagaa katika majivu, enyi wakubwa wa kundi. Siku za kuchinjwa kwenu na kusambazwa zinakaribia. Mutauawa kama kondoo dume wanene.


Kwa hiyo, muvae gunia, muomboleze na kulia; kwa maana Yawe hajaondoa hasira yake kali kwenu.


Wakikuuliza hivi: Kwa nini unaomboleza? Utawaambia: Ninaomboleza kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila mutu atavunjika moyo, mikono yao yote itaregea; kila mutu anayeishi atazimia na magoti yao yataregea. Habari hizo zinakuja kweli, nazo zinatimia. –Ni Bwana wetu Yawe anayesema hivyo.


Mutakapoyakimbia maangamizi ya inchi yenu, Misri itawakaribisha ninyi kwake, lakini makaburi yenu yanawangoja kule Memufisi. Michongoma itaota katika vyombo vyenu vya feza, miiba itajaa katika mahema yenu.


Enyi makuhani, muvae magunia kwa kuomboleza, mulie, enyi munaotumika kwenye mazabahu. Muingie katika hekalu muomboleze usiku kucha! Sadaka za chakula na kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Mungu.


Enyi walevi, muamuke na kulia; enyi walevi wa divai, mulalamike; zabibu zote za kutengeneza divai mupya zimeharibiwa.


Ole wenu wakaaji wa inchi za pembeni ya bahari, watu wanaoishi kule Krete! Yawe amesema juu yenu, enyi wakaaji wa Kanana, inchi ya Wafilistini: Mimi nitawaangamiza wala hakutabaki hata mukaaji mumoja!


Kila chungu katika Yerusalema na inchi ya Yuda kitatolewa kwa Yawe wa majeshi, kusudi wote wanaotoa sadaka waweze kuvitumia kwa kupikia nyama ya sadaka. Wakati ule, hakutakuwa muchuuzi yeyote katika hekalu la Yawe wa majeshi.


Akawaambia wachuuzi wa njiwa: “Muondoshe vile vitu hapa. Musifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!”


Basi, munisikilize sasa ninyi watajiri! Mulie na kuomboleza kwa sababu ya taabu itakayowapata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ