Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Zefania 1:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Siku hiyo, kutasikilika kilio kutoka Mulango wa Samaki, maombolezo kutoka Mutaa wa Pili, na mulio mukubwa kutoka katika milima. –Ni ujumbe wa Yawe.–

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Zefania 1:10
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hata hivyo, mufalme Daudi aliteka kikingio cha Sayuni, ni kusema muji wa Daudi.


Daudi alikaa kwenye kikingio hicho. Akakiita: “Muji wa Daudi.” Daudi akaongeza muji, akianzia uwanja wa Milo kuelekea ndani.


Kwa hiyo kuhani Hilkia, Ahikamu, Akibori, Safanu na Asahiya, wote walikwenda kuomba shauri kwa mwanamuke mumoja nabii jina lake Hulda aliyekuwa muke wa Salumu mwana wa Tikwa, mujukuu wa Harihasi, mutunza nguo za hekalu. Wakati ule, Hulda alikuwa anaishi katika mutaa wa pili wa Yerusalema, nao wakazungumuza naye.


Kisha Solomono akaanza kujenga nyumba ya Yawe katika Yerusalema juu ya mulima Moria ambapo Yawe alimutokea Daudi baba yake, pahali ambapo Daudi alikuwa amepachagua, kwenye kiwanja cha kupepetea ngano cha Ornani Muyebusi.


Kwa njia hii basi, Yawe akamwokoa mufalme Hezekia na wakaaji wa Yerusalema kutoka mukono wa Saniharibu mufalme wa Asuria, na kutoka mukono wa waadui zake wote. Akawapa maisha ya amani na wajirani zao wote.


Nyuma ya hayo, Manase akajenga ukuta mwingine upande wa inje wa muji wa Daudi, upande wa magaribi wa Gihoni, katika bonde, akauendelesha mpaka kwenye Mulango wa Samaki, akauzungusha Ofeli; akauinua juu sana. Pamoja na hayo, akaweka majemadari wa majeshi katika miji yote ya inchi ya Yuda yenye kuta.


Kwa hiyo Hilkia pamoja na wale wengine mufalme aliowatuma wakamwendea nabii Hulda muke wa Salumu, mwana wa Tokati, mujukuu wa Hasira, mulinzi wa nguo zilizotumika katika hekalu; (alikuwa anaishi katika Yerusalema katika mukoa wa pili); nao walizungumuza naye juu ya yaliyotokea.


Na kutoka pale, tukapitia kwenye Mulango wa Efuraimu, Mulango wa Yesana, Mulango wa Samaki, Munara wa Hananeli, Munara wa Mia moja mpaka kwenye Mulango wa Kondoo. Tulimalizia maandamano yetu kwenye Mulango wa Walinzi.


Nao watu wa ukoo wa Hasena wakajenga upya Mulango wa Samaki, wakatia miimo yake, milango, vyuma na vifungio vyake.


Tunanguruma kama dubu, tunaomboleza kama njiwa. Tunatazamia watu wanaofuata sheria ya Mungu, lakini hakuna, tunatazamia wokovu, lakini uko mbali nasi.


Na katika siku ya kenda ya mwezi wa ine, mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Zedekia, sehemu ya ukuta wa muji ilibomolewa.


Nilisikia sauti kama ya mwanamuke anayezaa, malalamiko kama ya mwenye kuzaa mutoto wa kwanza. Ilikuwa sauti ya Yerusalema akipumuapumua kwa uchungu, na kuinyooshanyoosha mikono yake, akisema: Ole wangu! Wanakuja kuniua!


Wakati maiti zao zitakapokuwa zimelala kati ya sanamu zao za miungu, na kwenye mazabahu zao juu ya kila mulima, chini ya kila muti wenye kivuli, chini ya kila muti wa mwalo wenye majani na popote walipotolea sadaka zenye harufu nzuri ya kuzipendeza sanamu zao za miungu. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Siku hiyo, nyimbo za nyumba ya kifalme zitakuwa maombolezo. –Ni ujumbe wa Yawe.– Kutakuwa maiti nyingi, nazo zitatupwa fasi zote kimyakimya.


Siku hiyo itakuwa siku ya kasirani, ni siku ya taabu na uchungu, siku ya giza na huzuni; siku ya uharibifu na maangamizi, siku ya mawingu na giza kubwa.


Munyamaze mbele ya Bwana wenu Yawe, maana siku ya Yawe iko karibu. Yawe ametayarisha sadaka, naye amekwisha kutakasa waalikwa wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ