Vyombo vyote vya kunywa divai vya mufalme Solomono vilikuwa vya zahabu, na vyombo vyote vilivyokuwa katika Nyumba ya Pori ya Lebanoni vilikuwa vya zahabu safi; hakuna kilichotengenezwa kwa feza maana madini ya feza haikuhesabiwa kuwa kitu wakati ule.
Ataunyanganya utajiri wako pamoja na biashara yako. Atazibomoa kuta zako na kuziangusha nyumba zako nzuri; mawe, mbao na udongo ulivyotumia kwa kujenga nyumba hizo watavitupa katika bahari.
Mali yako, biashara yako, na vitu vyako, waongozi wako wote katika chombo, wafundi wako wa mashua na wachuuzi wako, waaskari wako wote wanaokuwa kwako, pamoja na wasafiri wanaokuwa kwako, vyote vitaangamia ndani ya bahari, siku ile ya kuangamizwa kwako.
Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Tiro, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka mpaka Edomu. Hawakutii mapatano ya urafiki waliokuwa wamefanya.
Hapo, mupaka uligeuka kuelekea Rama na kufikia kwenye muji wa Tiro uliokuwa na kuta. Kisha ukageuka kuelekea Hosa na kuishia kwenye bahari ya Mediteranea. Miji mingine iliyokuwa katika eneo lile ni Maharabu, Akizibu,