Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




ZAKARIA 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Akaniuliza: Unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kinara cha taa cha zahabu. Juu yake kuna bakuli la mafuta na taa saba, na kila moja ina pahali pa kutilia tambi saba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




ZAKARIA 4:2
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

uzito wa vinara vya zahabu na taa zake, uzito wa kila kinara na taa zake kiasi cha feza ya kutengeneza kinara na taa zake kulingana na matumizi ya kila kinara;


Kila siku asubui na magaribi, makuhani wanamutolea sadaka za kuteketezwa na kumufukizia ubani wenye harufu nzuri, tena wanapanga mikate inayotolewa na Mungu juu ya meza ya zahabu safi, na kutunza kinara cha zahabu na kuwasha taa kila siku magaribi. Sisi tunayafuata maagizo ya Yawe, Mungu wetu, lakini ninyi mumemwacha.


Alitengeneza vinara kumi vya zahabu kama vile ilivyoagizwa, akaviweka katika baraza ya hekalu; vitano upande wa kusini, na vitano upande wa kaskazini.


uzi wa feza unakatika kikombe cha zahabu kinapondekana, mutungi wa maji unavunjikia kwenye chemichemi, gurudumu la kukokota maji linavunjika kwenye kisima,


Basi, Yawe akaniuliza: Yeremia! Unaona nini? Mimi nikamujibu: Ninaona tini. Zile nzuri ni nzuri sana, na zile mbaya ni mbaya sana hata hazifai kukuliwa.


Yule mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme alipeleka vibakuli, vyetezo, mabeseni, vyungu, vinara vya taa, vijiko vikubwa na mabakuli ya sadaka za vinywaji, vyombo hivyo vikiwa vya zahabu au vya feza.


Naye akaniuliza: Amosi, unaona nini? Nikamujibu: Ninaona timazi. Kisha Yawe akasema: Ninaweka timazi kati ya watu wangu Waisraeli. Sitavumilia tena maovu yao.


Yule malaika akaniuliza: Unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kitabu kinaruka katika anga; urefu wake ni metre kenda na upana wake ni metre ine na nusu.


Basi nikageuka kusudi nione yule aliyesema nami. Na wakati nilipogeuka nikaona vinara saba vya taa vilivyotengenezwa na zahabu.


Hii ndiyo maana ya lile fumbo juu ya zile nyota saba ulizoona katika mukono wangu wa kuume, na vile vinara saba vya zahabu: zile nyota saba ni wamalaika wa makanisa saba na vile vinara saba ni yale makanisa saba.


Umeme ulipiga tokea katika kiti kile, na makelele na ngurumo ya radi vilisikilika. Mbele ya kiti kile kulikuwa kukiwaka mienge saba, na hizo ndizo zile roho saba za Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ