Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




ZAKARIA 13:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mutu yeyote akijidai kuwa nabii, baba na mama yake waliomuzaa watamwambia: “Unapaswa kufa maana unasema uongo kwa jina la Yawe.” Na wale wazazi wake watamuchoma kisu akiwa anatabiri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




ZAKARIA 13:3
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mimi nimeyasikia maneno waliyosema hao manabii wanaotabiri uongo kwa jina langu, wakisema: Nimeota ndoto, nimeota ndoto!


Tena nabii au kuhani, au mutu yeyote atakayesema: “Muzigo wa Yawe”, nitamwazibu pamoja na jamaa yake yote.


Basi, nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania: Sikiliza, Hanania. Yawe hakukutuma, nawe unawafanya watu hawa waamini uongo.


basi, ninyi hamutapata tena maono madanganyifu, wala hamutatabiri tena. Nitawaokoa watu wangu toka katika mikono yenu. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Na ikiwa nabii yule akidanganyika na kusema kitu, basi mimi Yawe nimemupotosha. Nami nitanyoosha mukono wangu kwa kumwondoa nabii yule kutoka kwa watu wangu Waisraeli.


naye akaniambia: Wewe mwanadamu! Hapa ndipo pahali pa kiti changu cha kifalme, pahali ninapoweka miguu yangu. Nitakaa kati ya watu wa Israeli milele. Na Waisraeli hawatalichafua jina langu, wao wenyewe, wala wafalme wao kwa kuziabudu sanamu au kuzika maiti za wafalme wao pahali hapa.


“Yeye anayemupenda baba yake au mama yake kuliko mimi, hastahili kuwa wangu, na yeyote anayemupenda mwana wake au binti yake kuliko mimi hastahili kuwa wangu vilevile.


“Mutu anayenifuata, atakuwa kweli mwanafunzi wangu kama akinipendelea mimi kuliko baba na mama yake, muke na watoto wake, wakaka na wadada zake. Na zaidi ya hii hapaswi kujipendelea yeye mwenyewe vilevile.


Kwa hiyo basi, tangu sasa hatumuhesabu tena mutu yeyote kufuatana na hali ya kimutu. Hata ikiwa tulimuhesabu Kristo kufuatana na hali ya kimutu, kwa sasa hatumuhesabu tena kufuatana na hali ile.


Lakini nabii yeyote atakayesema kwa jina la miungu mingine, au atakayejaribu kusema neno kwa jina langu wakati mimi sikumwambia aseme, huyo nabii atakufa.’


Walawi waliacha wazazi wao, wakawasahau wandugu zao, hawakuwatambua hata watoto wao, maana walifuata amri zako, na kushika agano lako.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ