Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




ZAKARIA 10:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yawe anasema hivi: Nimewaka hasira juu ya hao wachungaji, nami nitawaazibu hao watawala. Mimi Yawe wa majeshi, nitalitunza kundi langu, ukoo wa Yuda. Nitawafanya kuwa farasi wangu hodari wa vita.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




ZAKARIA 10:3
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kila mara baragumu inapopigwa, yeye anatoa sauti; anasikia harufu ya vita toka mbali, anasikia mushindo wa majemadari wakitoa amri kwa makelele.


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


Farasi anatayarishwa kwa vita, lakini ushindi unaletwa na Yawe.


Wewe ee mupenzi wangu, ninakulinganisha na farasi dume wa magari ya Mufalme wa Misri.


Wakati Yawe atakapomaliza kazi zake zote kwenye mulima Sayuni na katika Yerusalema, atamwazibu mufalme wa Asuria, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.


Siku ile Yawe ataliazibu jeshi la anga vilevile na wafalme wa dunia.


Nami Yeremia nikasema: Wachungaji wamekuwa wajinga, hawakuuliza shauri kwa Yawe; kwa sababu hiyo, hawakufanikiwa, na kondoo wao wote wamesambaa.


Ndiyo, Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitawaazibu watu hao. Vijana wao watauawa kwa upanga; watoto wao wanaume na wanawake watakufa kwa njaa.


Hiyo miaka makumi saba itakapopita, nitamwazibu mufalme wa Babeli pamoja na taifa lake. Nitaiangamiza inchi hiyo ya Wababeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitafanya hivyo kwa sababu ya uovu wao na kuifanya inchi ibaki mabomoko hata milele.


Muomboleze, enyi wachungaji; mulie na kugaagaa katika majivu, enyi wakubwa wa kundi. Siku za kuchinjwa kwenu na kusambazwa zinakaribia. Mutauawa kama kondoo dume wanene.


Watu wangu walikuwa kama kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha, wakawageuza kuelekea kwenye milima; walitembea toka mulima mpaka kilima, wakasahau makao yao.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe nitawatafuta kondoo wangu na kuwatunza.


Kama muchungaji anavyowatafuta kondoo wake waliosambazwa, ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawarudisha kutoka kila pahali waliposambazwa kwa siku yenye mawingu ya hatari na giza nene.


Wewe mwanadamu! Toa unabii juu ya wachungaji wa inchi ya Israeli. Uwaambie hao wachungaji kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ole kwenu ninyi wachungaji wa inchi ya Israeli, munaojikulisha ninyi wenyewe tu! Haiwapasi wachungaji kuwakulisha kondoo?


Atawashawishi kwa werevu wale walioasi agano, lakini watu wanaokuwa waaminifu kwa Mungu wao watasimama imara na kutenda.


Yawe anasema hivi: Katika siku ile ya karamu yangu, nitawaazibu wakubwa wa watu hao, vilevile na wana wa mufalme pamoja na wote wanaoiga desturi za kigeni.


Inchi ya pembeni ya bahari itakuwa makao ya mabaki ya ukoo wa Yuda. Watachunga nyama wao kule. Nyumba za muji wa Askeloni zitakuwa pahali pao pa kulala. Maana mimi Yawe, Mungu wao nitawakumbuka na kuwarudishia hali yao njema.


Ole wake muchungaji mupumbafu, ambaye anawaachilia kondoo wake! Upanga uukate mukono wake, na jicho lake la kuume liongolewe! Mukono wake upooze, jicho lake la kuume lipofuke.


“Asifiwe Bwana, Mungu wa Waisraeli, maana amewasaidia watu wake na kuwakomboa.


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


Kisha, Naomi akapata habari kwamba Yawe alikuwa amewabariki watu wake kwa kuwapa chakula. Basi, akaondoka kutoka Moabu kurudi kwao, pamoja na wakwe zake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ