3 Nitafurahi na kushangilia kwa ajili yako; nitaliimbia sifa jina lako, ewe Mungu Mukubwa.
Ulipowakaripia, ee Mungu wa Yakobo, farasi na wapanda-farasi walipooza.
Ulinde kijiti ulichokipanda kwa mukono wako; hicho kichipukizi ulichokomalisha wewe mwenyewe.
Wewe umemufanya Yawe kuwa kimbilio lako; Mungu anayekuwa juu kuwa tegemeo lako.
Ni vizuri kukushukuru, ee Yawe, kuliimbia jina lako sifa, ee Mungu Mukubwa.
Tangu zamani hakuna aliyepata kusikia kwa masikio yake wala kumwona Mungu anayekuwa kama wewe, anayetenda mambo kama hayo kwa ajili ya wale wanaomutegemea!
Azabu yao itakuwa kuangamizwa kwa milele, na kutengwa mbali na uso wa Bwana na mbali na utukufu wa uwezo wake,
Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.