Kwa vile umefanya mipango juu yangu na nimesikia majivuno yako, nitatia ndoana yangu ndani ya pua yako, na lijamu yangu ndani ya kinywa chako. Nitakurudisha katika njia ileile uliyokuja ndani yake.
Kwa vile umefanya mipango juu yangu na nimesikia majivuno yako, nitatia ndoana yangu ndani ya pua yako, na lijamu yangu ndani ya kinywa chako. Nitakurudisha katika njia ileile uliyokuja ndani yake.
Basi Pilato alipoona kwamba hataweza kufanya kitu, isipokuwa tu kuongeza fujo, akatwaa maji na kunawa mikono yake mbele ya watu wote, akisema: “Lazima ya damu ya mutu huyu isikuwe juu ya kichwa changu! Maneno haya yanawaangukia.”
Lakini Wayuda wakajaa na wivu, hata wakakusanya watu wamoja wa ovyo ovyo waliowakuta kwenye nafasi za makutano, na kufanya kikundi. Kisha wakafanya fujo katika muji wote. Wakashambulia nyumba ya Yasoni, wakiwatafuta Paulo na Sila kusudi wawapeleke mbele ya watu.
Muji wote ukajaa fujo na watu wakakusanyika pale mbiombio. Wakamukamata Paulo na kumukokotea mpaka inje ya hekalu, na mara moja wakafunga milango yake.
Ugomvi ulipozidi sana, jemadari akaogopa kwamba watu wale watamurarua Paulo. Kwa hiyo akaamuru waaskari waende katikati ya mukutano ule na kumwondosha Paulo kwa kinguvu katikati yao na kumurudisha ndani ya upango wa waaskari.