4 Wapumbazike kwa haya, hao wanaofurahia kunizomea!
Lakini wanaotaka kuona kwamba sina kosa, wakuwe na furaha tele, waseme siku zote: “Yawe ni mukubwa! Anapendezwa na kumupatia mutumishi wake uheri.”
Hao wanaonisimanga, wafezeheke kwa kushindwa kwao!
Ee Mungu, uwaazibu kwa makosa yao, waanguke katika mipango yao wenyewe; uwafukuze inje kwa sababu ya zambi zao nyingi, kwa sababu wamekuasi wewe.
Mufurahi kwa sababu ya Yawe, enyi watu wa haki; mumushukuru kwa ajili ya utakatifu wake.
Nitafurahi sana kwa sababu ya Yawe, nafsi yangu itashangilia kwa sababu ya Mungu wangu. Maana amenivalisha nguo ya wokovu, amenifunika kanzu ya haki, kama bwana arusi anavyojipamba kwa shada la maua, kama bibi arusi anavyojipamba kwa ushanga wake.
Yawe ni muzuri kwa wanaomutegemea, kwa wote wanaomutafuta.
Kweli, kweli ninawaambia: mutalia na kusikitika, lakini watu wa dunia watafurahi. Mutahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.