5 Watu wengi kuliko nywele zangu wananichukia. Wana nguvu sana hao wanaotaka kuniua, hao wanaonishambulia kwa mambo ya uongo. Nirudishe kitu ambacho sikuiba?
Wewe unajua kabisa moyo wangu; umenifikia usiku kunichunguza, umenitia katika majaribu; haukuona uovu ndani yangu, sikusema kitu kisichofaa.
Yananifundisha mimi mutumishi wako; kuyafuata kunaniletea zawadi kubwa.
Usiwaache waadui hao wabaya wanisimange, hao wanaonichukia bure, wafurahie mateso yangu.
Nimefunikwa kabisa na zambi zangu, zinanilemea kama muzigo muzito sana.
Nimeregea na kupondekanapondekana; ninaugua kwa kusongwa katika moyo.
Maana, mimi ninayaona matendo yao yote, hakuna hata moja linalofichama mbele yangu. Maovu yao yote ni wazi mbele yangu.