Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Zaburi 69:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ninazama ndani ya matope mengi, hakuna pahali pa kuweka miguu. Nimetumbukia kwenye shimo refu la maji, ninachukuliwa na maji mengi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Zaburi 69:3
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini waovu macho yao yatafifia, njia zote za kutorokea zitawapotea; tumaini lao la mwisho ni kukata roho!


Macho yangu ni mekundu kwa sababu ya kulia, kope zangu zimekuwa nyeusi sana,


Macho yangu yanafifia nikingojea uniokoe, nikingojea utimize uliyoahidi.


Macho yangu yanafifia nikingojea ulichoahidi. Ninauliza: “Utakuja wakati gani kunifariji?”


Nimekwisha kama maji yaliyomwangika; mifupa yangu yote imeteguka; moyo wangu ni kama inta, unayeyuka ndani yangu.


Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Mbona uko mbali sana kwa kunisaidia, mbali na maneno ya kilio changu?


Ukamilifu na usawa vinanikinga, maana ninakutumainia wewe.


Kweli, kila mutu anapita kama kivuli; masumbuko yake yote ni bure tu; anakusanya mali, hajui atakayeipata!


Aliniondoa katika shimo la hatari, alinitoa katika matope mengi, akanisimamisha salama juu ya mulima, na kuziimarisha hatua zangu.


Huko kwa wafu hakuna anayekukumbuka; katika kuzimu ni nani anayeweza kukusifu?


Matusi yamevunja moyo wangu, nami nimekata tamaa. Nimetafuta kitulizo lakini sikupata, nimetafuta wa kunifariji lakini sikumupata.


Umenitupa mbali katika shimo la wafu, katika giza kubwa.


Ninalia kama mbaruwayi, ninaugua kama njiwa. Macho yangu yamefifia kwa kuangalia juu. Ee Bwana, ninateseka; ukuwe wewe usalama wangu!


Macho yangu yamevimba kwa kulia, roho yangu imechafuka, moyo wangu una huzuni nyingi, kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu, kwa sababu watoto wachanga na wale wanaonyonya wanazimia katika barabara za muji.


Kisha, Yesu akiwa anajua kwamba mambo yote yametimia, akasema hivi kusudi Maandiko Matakatifu yatimie: “Ninasikia kiu.”


Watoto wenu wanaume na wanawake watatolewa kwa watu wengine nanyi mutakodoa macho muchana kutwa kuwatazamia warudi, lakini hamutakuwa na nguvu ya kufanya chochote.


Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ