Mbona ninahuzunika hivyo katika moyo? Kwa nini ninahangaika hivyo ndani mwangu? Nitamutumainia Mungu, nitamusifu tena yeye anayekuwa musaada wangu na Mungu wangu.
Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.
Kwa hiyo, ee Mungu, usikilize malalamiko yangu na maombi yangu mimi mutumishi wako. Kwa ajili ya heshima yako, ulionee tena hekalu lako lililoharibika huruma.
na kusema: “Wewe mutoto wa Shetani unayejaa udanganyifu na ukorofi wa kila namna! Wewe usiyependa kuona jambo la haki! Wewe hauchoki na kugeuza maneno ya ukweli ya Bwana!
Mutu huyu alikuwa amefundishwa Njia ya Bwana, naye alitangaza kwa bidii sana na kufundisha kwa ukweli habari za Yesu. Lakini alikuwa akijua tu ubatizo wa Yoane.
Wakati ule, kanisa lilikuwa na amani katika Yudea yote, Galilaya na Samaria. Vilevile lilizidi kupata nguvu na kuendelea kumwogopa Bwana, nalo liliongezeka kwa musaada wa Roho Mutakatifu.