Hiyo itakuwa kwa ajili ya Walawi, kwa sababu hawana fungu wala urizi wao kati yenu, nao wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu, watakuja kula na kushiba. Mufanye hivi naye Yawe, Mungu wenu, atawabariki katika kazi zenu zote munazofanya kwa mikono yenu.
Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.
Basi mama mukwe wake akamwuliza: “Uliokota wapi haya yote? Ulikuwa katika shamba la nani? Abarikiwe yule aliyekutendea wema.” Hapo Ruta akamwambia Naomi kwamba alikuwa akifanya kazi katika shamba la mutu aliyeitwa Boazi.