4 Hata hivyo, wewe ni mutakatifu; wewe unatawala na kusifiwa na Waisraeli.
Abramu alimwamini Yawe, naye Yawe akamuhesabu kuwa mwenye haki.
Naye akamwuliza: “Jina lako nani?” Yeye akamujibu: “Yakobo.”
Waimbaji na wapiga baragumu wote pamoja walitoa sauti kwa pamoja na matoazi na vyombo vingine vya muziki, wakimusifu Yawe wakiimba: “Yeye ni muzuri. Wema wake unadumu milele.” Wakati ule nyumba ya Yawe ikajazwa na wingu.
Waisraeli walipoona tendo hilo la ajabu Yawe alilofanya mbele ya Wamisri, wakamwogopa. Wakamwamini Yawe na Musa mutumishi wake.