6 Wenye kiburi wamenitegea mitego, wametandika kamba kama wavu, wameficha mitego katika njia wanikamate.
Ninasikia watu wakinongonezana; kuna vitisho kila upande. Wanafanya shauri baya juu yangu, wanafanya mipango ya kuniua.
Ninamwambia Mungu: “Wewe ni Bwana wangu; sina uheri wowote isipokuwa wewe.”
Nikiangalia kwa kuume kwangu na kungojea, ninaona hakuna mutu wa kunisaidia; sina tena nafasi ya kukimbilia, hakuna mutu anayenijali.
Wewe, ee Yawe, ndiwe hitaji langu lote; ninaahidi kushika maneno yako.
Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.
Yawe ndiye sehemu yangu, hivyo nitamuwekea tumaini langu.
Zaburi ya Daudi. Usikie maombi yangu, ee Yawe! Ulitegee ombi langu sikio, maana wewe ni mwaminifu; unijibu kwa sababu ya haki yako.
Ee Bwana, usikie sauti yangu, ulitegee ombi langu sikio.
Ninamupenda Yawe, kwa maana ananisikia, maana amesikia kilio cha ombi langu.
utaweza kumwambia Yawe: “Wewe ni kimbilio langu ninamojificha, Mungu wangu ninayemutumainia!”
Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.
Waadui wamenitegea wavu waninase, nami ninaugua kwa huzuni. Wamenichimbia shimo katika njia yangu, lakini wao wenyewe wametumbukia humo.
Roho yangu inaporegea kabisa, yeye yuko, anajua mwenendo wangu. Waadui wamenitegea mitego katika njia ninayopita.
Kilio kisikilike katika nyumba zao, utakapowaletea kundi la wanyanganyi kwa rafla. Maana wamechimba shimo waninase; wameitegea miguu yangu mitego.