Mungu akawabariki na kuwaambia: “Muzae, muongezeke, na mujaze inchi na kuitawala. Mutawale samaki wa bahari, ndege wa anga, na kila kiumbe chenye uzima kinachotembea katika dunia.”
Esau alipoinua macho na kuwaona wale wamama na watoto, akauliza: “Ni wa nani hawa unaokuwa nao?” Yakobo akamujibu: “Hawa ni watoto ambao Mungu, kwa neema yake, amenijalia mimi mutumishi wako.”
Wana wa Ulamu walikuwa watu mashujaa sana wa vita, na wapiga upinde hodari. Alikuwa na wana na wajukuu wengi, jumla yao walikuwa mia moja makumi tano. Hao wote waliotajwa hapo juu walikuwa wa ukoo wa Benjamina.
Yeye alikuwa na wana makumi tatu na wabinti makumi tatu. Nao wabinti zake aliwaoesha inje ya ukoo wake, na wana aliwaoea wabinti makumi tatu kutoka inje ya ukoo wake. Ibusani alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka saba.