Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yuda 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Maana kuna watu wasiomuheshimu Mungu waliojiingiza kwa siri kati yetu. Watu hawa wanapotosha ujumbe wa neema ya Mungu wetu kusudi wapate kufanya uasherati na kumukana Yesu Kristo, anayekuwa peke yake Kiongozi na Bwana wetu. Tangia zamani Maandiko Matakatifu yamejulisha hukumu ile itakayowapata watu hawa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yuda 1:4
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mawimbi ya kifo yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinishambulia,


Heri mutu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi, wala kukusanyika na wenye kuzarau;


Kwa Mungu peke yake ninapata utulivu, wokovu wangu unatoka kwake.


Lakini siku moja usiku, wote walipokuwa wakilala usingizi, adui wa mutu yule akakuja na kupanda nyasi katikati ya ngano; kisha akajiendea.


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


Tumesikia kwamba watu fulani waliotoka huku kwetu pasipo ruhusa yetu wamewasumbua ninyi na maneno na kuwatia katika wasiwasi.


ijapokuwa wandugu wamoja wa uongo waliojiunga nasi kwa kisirisiri walitaka kumutahiri. Watu hao walijiingiza katika kikundi kusudi wapate kupeleleza jinsi tunavyoishi katika uhuru kutokana na kuungana kwetu na Yesu Kristo. Walitaka kututia katika maisha ya kitumwa.


Wandugu, ninyi muliitwa na Mungu kusudi mukuwe watu huru. Basi musitumie uhuru huu kuwa ruhusa ya kutimiza tamaa za mwili, lakini musaidiane kwa upendo.


Basi, hatutakuwa tena kama watoto, tukipeperushwa na kuvutwa na mafundisho ya kila aina yanayoletwa na watu wanaodanganya wengine na kuwapotosha kwa mayele yao.


Kama mutu asipotunza wandugu zake na hasa zaidi watu wa jamaa yake mwenyewe, huyu amekana imani yake naye ni mubaya kuliko mupagani.


Kama tunaendelea kuvumilia, tutatawala pamoja naye vilevile. Kama tunamukana, naye atatukana vilevile.


Kwa maana kati yao kuna wamoja wanaojiingiza katika nyumba za watu na kuwashawishi wanawake wajinga wanaolemewa na mizigo ya zambi na kuvutwa na tamaa za namna nyingi.


Muishi kama watu wanaokuwa na uhuru, lakini musitumie uhuru wenu kwa kufunika ubaya, lakini muishi kama watumwa wa Mungu.


Tena imeandikwa kwamba: “Jiwe lile ni la kukwalisha watu, nalo ni la kuwaangusha.” Wamejikwaa kwa sababu hawakuamini neno la Mungu, na hivi ndivyo walivyopanga kwa ajili yao tangu mwanzo.


Ni kama vile Maandiko haya Matakatifu yanavyosema: “Ikiwa hata kuokolewa kwa mwenye haki ni kugumu; itakuwa namna gani kwa mwovu na mwenye zambi?”


Na zaidi atawaazibu wale wanaoishi kufuatana na tamaa mbaya za kimwili na kuzarau mamlaka ya Mungu. Walimu wale wa uongo ni wenye kiburi, wenye kujivuna, nao hawaogopi kutukana viumbe vitukufu vya mbinguni.


Mungu alimwokoa Loti, mutu wa haki, aliyehuzunishwa sana na mwenendo mubaya wa wale watu waovu.


Lakini kwa nguvu ya neno lile lile, mbingu na dunia za sasa zimewekwa akiba kwa kuteketezwa kwa moto. Zinalindwa kwa ajili ya Siku ile ambayo watu wabaya watahukumiwa na kuangamizwa.


Ni nani anayekuwa musema uongo? Ni yule anayekana kwamba Yesu si Kristo. Huyu ndiye mupinga Kristo, kwa maana anamukana Baba na Mwana.


Atakuja kuwahukumu wote na kuwaazibu watu wabaya wasiomwogopa Mungu, kwa ajili ya matendo yao yote mabaya waliyotenda, na kwa ajili ya maneno yote mabaya wenye zambi hawa waliyosema juu yake.”


Wao waliwaambia: “Katika siku za mwisho, kutakuja watu watakaowachekelea, wakiishi kwa kufuata tamaa zao mbaya.”


Ewe Bwana, hakuna asiyekuogopa, wala hakuna asiyekutukuza, kwa maana wewe peke yako ndiwe mutakatifu. Mataifa yote yatakuja kukuabudu, kwa maana matendo yako ya haki yameonyeshwa wazi.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ