Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yuda 1:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Watu hawa wanaendelea kunungunika na kuteta wengine. Wanaishi kufuatana na tamaa zao mbaya. Wanasema maneno ya majivuno na kujipendekeza kwa watu kusudi wapate faida toka kwao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yuda 1:16
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sitamupendelea mutu yeyote wala kutumia maneno ya kubembeleza mutu,


Yeye hawapendelei wakubwa, wala kuwajali watajiri kuliko wamasikini, maana wote hao ni kazi ya mikono yake.


Walinungunika ndani ya hema zao, wala hawakumusikiliza Yawe.


Hao hawana huruma yoyote ndani ya moyo; wamejaa maneno ya kujivuna.


Wanawachekelea wengine na kusema mabaya; wanajivuna na kufanya mipango ya utesaji.


Si vizuri kumubagua mutu. Watu wanafanya mabaya hata kwa ajili ya mukate.


Waliopotoka katika roho watapata maarifa na wenye kunungunika watakubali kufundishwa.


Unapotoa hukumu uamue kwa haki, usimupendelee masikini wala kumwogopa mwenye cheo. Lakini hukumu mwenzako kwa haki.


Wale watu ambao Musa aliwatuma kwenda kupeleleza ile inchi waliorudi na kusababisha watu wamunungunikie Yawe kwa kuleta habari ya uongo juu ya inchi,


Si Haruni tu munayemunungunikia, wewe na kundi lako, lakini kwa kweli munamwasi Yawe.


Wafarisayo na walimu wa Sheria wakaanza kunungunika, wakisema: “Mutu huyu anawakaribisha watenda mabaya na kula pamoja nao!”


Watu wote walioona hayo wakaanza kunungunika wakisema: “Amekwenda kupanga kwa mutenda maovu!”


Wafarisayo na walimu wa Sheria wa kikundi chao wakawanungunikia wanafunzi wake, wakisema: “Kwa sababu gani munakula na kunywa pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”


Basi Wayuda wakaanza kunungunika kwa sababu Yesu alisema kwamba yeye ni mukate ulioshuka toka mbinguni.


Yesu akafahamu kwamba wanafunzi wake wananungunika juu ya neno hili; basi akawauliza: “Neno hili linawakwaza?


Musinungunike kama vile wamoja kati yao walivyofanya hata malaika mwangamizaji akawateketeza.


Mambo ninayotaka kusema ni haya: muishi chini ya uongozi wa Roho Mutakatifu, nanyi musitimize tamaa za kimwili.


Nao watu wa Kristo Yesu wameua hali yao ya kimutu pamoja na vifungo vyao vyote na tamaa zote mbaya.


Mulinungunika ndani ya mahema yenu mukisema: ‘Yawe anatuchukia na ndiyo maana alitutoa katika inchi ya Misri. Alitaka kututia katika mikono ya Waamori kusudi atuangamize.


Mufanye kila kitu bila manunguniko wala mabishano,


bila kujiachilia kutawaliwa na tamaa mbaya kama vile wapagani wasioamini Mungu.


na magomvi yasiyokuwa na mwisho ya watu wenye akili iliyokwisha kupotoka hata wamesahau ukweli kabisa. Ndio wale wanaozani kwamba dini ni njia ya kupata utajiri.


Maana kutakuja wakati watu watakapokataa kusikiliza mafundisho ya kweli, lakini watafuata tamaa zao wenyewe wakijitafutia walimu wengi kwa kuwafundisha mambo yale wanayotamani kusikia.


Kama watoto wenye utii, musiachilie maisha yenu kutawaliwa na tamaa mbaya mulizokuwa nazo zamani wakati mulipokuwa mukiishi katika ujinga.


Wapendwa wangu, ninawasihi ninyi, kama vile wageni na wasafiri hapa katika dunia, muepuke tamaa za mwili zinazopigana na roho.


Sasa, musiishi tena kufuatana na tamaa za kimutu, lakini muishi kufuatana na mapenzi ya Mungu kwa muda unaowabakilia kwa kukaa katika dunia.


Na zaidi atawaazibu wale wanaoishi kufuatana na tamaa mbaya za kimwili na kuzarau mamlaka ya Mungu. Walimu wale wa uongo ni wenye kiburi, wenye kujivuna, nao hawaogopi kutukana viumbe vitukufu vya mbinguni.


Kwa maana kwa masemi yao ya kujivuna na yasiyokuwa na maana, na kwa njia ya tamaa zao mbaya za kimwili, wanawavuta watu ambao wanaanza kuwaepuka, na wale wanaoishi katika udanganyifu.


Mbele ya yote, mujue kwamba katika siku za mwisho kutakuja watu watakaoishi kufuatana na tamaa zao wenyewe. Watawachekelea ninyi


Atakuja kuwahukumu wote na kuwaazibu watu wabaya wasiomwogopa Mungu, kwa ajili ya matendo yao yote mabaya waliyotenda, na kwa ajili ya maneno yote mabaya wenye zambi hawa waliyosema juu yake.”


Wao waliwaambia: “Katika siku za mwisho, kutakuja watu watakaowachekelea, wakiishi kwa kufuata tamaa zao mbaya.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ