Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 9:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Wakamujibu: “Sisi, watumishi wako, tumetoka inchi ya mbali na tumekuja kwa maana tumesikia sifa za jina la Yawe, Mungu wenu. Tulipata habari za utukufu wake na yote aliyoyafanya katika inchi ya Misri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 9:9
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Hata wakati mugeni asiyekuwa mumoja wa watu wako Waisraeli akikuja kutoka inchi ya mbali kwa ajili ya jina lako,


Walawi, ni kusema Yesua, Kadimieli, Bani, Hasabuea, Serebia, Hodia, Sebania na Petahia, wakawaambia watu: Musimame na kumusifu Yawe, Mungu wenu. Mumusifu milele na milele! Na watu wakasifu jina lako tukufu, ambalo linatukuka kuliko baraka na sifa zote.


Wote musifu jina la Yawe, maana jina lake peke yake linatukuzwa; utukufu wake unapita dunia na mbingu.


Jina lake tukufu litukuzwe milele; utukufu wake ujae katika ulimwengu wote! Amina, Amina!


Alifanya maajabu mbele ya babu zao, katika mbuga za Soani kule Misri.


Wafezeheke na kuhangaika milele, waangamie kwa haya kabisa.


Watu wa mataifa wamesikia hayo wakatetemeka; Wafilistini wamepatwa na kitisho.


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Sasa utayaita mataifa usiyoyajua, watu wa mataifa yasiyokutambua watakuja mbio kwenu, kwa sababu yangu mimi Yawe, Mungu wako; kwa sababu yangu mimi Mutakatifu wa Israeli niliyekufanya wewe upate utukufu.


Nitaweka kati yao kitambulisho cha uwezo wangu. Watakaookolewa kati yao nitawapeleka kwa watu wa mataifa kule Tarsisi, Puti, Ludi, inchi zenye wafundi wa kupiga upinde; watakwenda vilevile Tubali na Ugriki na katika visanga vya mbali ambapo watu hawajapata kusikia habari zangu wala kuuona utukufu wangu. Wale wajumbe wangu watautangaza utukufu wangu katika mataifa hayo.


Sasa basi, ukiwaua watu wako wote kwa mara moja, mataifa ambayo yamekwisha kusikia sifa zako yatasema:


Musa akatuma wajumbe kutoka Kadesi kwa mufalme wa Edomu akamwambia: Ndugu yako Israeli anasema hivi: Wewe unajua taabu zote tulizozipata.


Maana pepo walitoka ndani ya watu wengi wakilalamika kwa sauti kubwa, na watu wengi wenye kupooza pamoja na viwete waliponyeshwa vilevile.


Wakaaji wa muji huo wakitaka amani na kujitoa kwenu, basi watu wote wanaokuwa humo watawatumikia na kufanya kazi za kulazimishwa.


Ndivyo mutakavyoitendea miji yote ambayo iko mbali na inchi mutakayorizi.


Tumesikia yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori waliokuwa ngambo ya muto Yordani, mufalme Sihoni wa Hesiboni na mufalme Ogi wa Basani aliyekaa kule Astaroti.


Siku tatu nyuma ya kufanya agano nao, Waisraeli wakagundua kwamba watu hao walikuwa jirani zao na waliishi kati yao.


Basi, Waisraeli wakafunga safari, nyuma ya siku ya tatu wakafika katika miji yao. Miji hiyo ilikuwa Gibeoni, Kefira, Beroti na Kiriati-Yearimu.


Wakamujibu Yoshua: “Tuliambiwa kwamba kwa hakika Yawe, Mungu wenu, alimwamuru mutumishi wake Musa awaangamize wakaaji wote wa inchi hii na kuwapa ninyi inchi hii ikuwe mali yenu. Kwa hivyo, tuliogopea maisha yetu na ndipo tukafanya jambo hili.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ