Kwa hiyo mukubwa wa nyumba ya mufalme na musimamizi wa muji, wakishirikiana na viongozi wengine na walinzi, wakamupelekea Yehu ujumbe huu: “Sisi ni watumwa wako, na tuko tayari kufanya lolote unalosema. Lakini hatutamuweka mutu yeyote kuwa mufalme. Fanya unavyotaka.”
Wagibeoni wakapeleka ujumbe kwa Yoshua kule katika kambi Gilgali, wakamwambia: “Tafazali, usitutupilie sisi watumishi wako. Ukuje mbio utusaidie na kutuokoa kwa maana wafalme wote wa Waamori kutoka inchi ya milima wamekuja kutushambulia.”
Halafu wazee wetu na wanainchi wote wa inchi yetu, wakatuambia, tutayarishe posho ya safari, tukuje kukutana nanyi na kuwaambia kwamba sisi ni watumishi wenu. Tafazali mufanye agano nasi.
Lakini kutokea siku hiyo, Yoshua akawafanya hao kuwa wakata - kuni na wachota - maji kwa ajili ya Waisraeli wote na kwa ajili ya mazabahu ya Yawe, popote pale Yawe alipochagua mpaka hivi leo.