na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
Hakuna muji ambao ulifanya mapatano ya amani na Waisraeli, isipokuwa Gibeoni tu, ambamo Wahivi waliishi. Waisraeli waliiteka miji mingine yote kwa kupigana vita.
Wafalme wote waliokuwa ngambo ya muto Yordani katika inchi ya milima na kwenye mabonde na eneo lote la pembeni ya bahari ya Mediteranea kuelekea Lebanoni, Wahiti, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi na Wayebusi waliposikia habari za Waisraeli,
Na kwa upande wenu niliwaamuru musifanye agano na wenyeji wa inchi hii na kwamba mazabahu zao mutazibomoa. Lakini ninyi hamukuitii amri yangu. Kwa nini mambo haya?
Aliacha mataifa ya watu hawa: wakubwa watano wa Wafilistini, Wakanana wote, Wasidoni na Wahivi waliohamia katika milima ya Lebanoni kutoka mulima Bali-Hermoni mpaka kufikia Hamati.