Nyuma ya mambo yale, Daudi alimwomba Yawe shauri, akasema: “Niende kwenye muji mumoja kati ya miji ya Yuda?” Yawe akamwambia: “Kwenda!” Daudi akamwuliza: “Niende katika muji gani?” Yawe akamujibu: “Kwenda kwenye muji wa Hebroni.”
Kisha, nikatoa maagizo kuwa sisi wote tufike karibu na muto Ahara kusudi tufunge kula chakula na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wetu na kumwomba atulinde na kutuongoza katika safari yetu pamoja na watoto wetu.
Kwenye kifuko hicho utatia mawe ya shauri yaninginie kwenye kifua cha Haruni kila mara anapokuja mbele yangu. Wakati ule anapaswa kila mara kuvaa kifuko kile, kusudi aweze kutambua mapenzi yangu juu ya Waisraeli.
Yeye atamutegemea kuhani Eleazari ambaye atamujulisha mapenzi yangu kwa kutumia jiwe la shauri. Kwa njia hii, Eleazari atamwongoza Yoshua na Waisraeli wote wanapotoka na wanapoingia.
Waisraeli wakaenda Beteli kuomba shauri kwa Mungu, wapate kujua kabila ambalo litakwenda kwanza kupigana na watu wa kabila la Benjamina. Yawe akataja kabila la Yuda liende kwanza.
Finehasi mwana wa Eleazari mwana wa Haruni alikuwa na kazi ya kutumika mbele yake. Waisraeli wakamwuliza Yawe: “Twende tena kupigana na wandugu zetu, watu wa kabila la Benjamina?” Yawe akawaambia: “Muende. Kesho nitawatia katika mikono yenu.”