Yoshua 9:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
10 Tumesikia yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori waliokuwa ngambo ya muto Yordani, mufalme Sihoni wa Hesiboni na mufalme Ogi wa Basani aliyekaa kule Astaroti.
Katika mwaka wa kumi na ine, mufalme Kedorilaomeri na wale wafalme wenzake wakakuja na kuwashinda watu wa Refaimu kule Astaroti-Karnaimu, Wazuzi kule Hamu, Waemi kule Sawe-Kiriataimu,
Alifanya hivyo kisha Yawe kumushinda mufalme Sihoni wa Waamori ambaye alikuwa anakaa katika muji wa Hesiboni, na mufalme Ogi wa Basani ambaye alikuwa anakaa katika muji wa Astaroti na Edirei.
“Lakini Sihoni, mufalme wa Hesiboni, hakuturuhusu tupite katika inchi yake. Yawe, Mungu wenu, akamufanya akuwe na kichwa kigumu na mugumu wa moyo, kusudi tumushinde na kutwaa inchi yake ambayo tunairizi mpaka leo.
nusu ya Gileadi, Astaroti, Edirei, ambayo ilikuwa ya mufalme Ogi wa Basani. Nusu ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, eneo hili walipewa kulingana na ukoo zao.
Maana tumesikia jinsi Yawe alivyoyakausha maji ya bahari Nyekundu mbele yenu mulipotoka inchi ya Misri, na jinsi mulivyowatendea wafalme wawili wa Waamori waliokuwa ngambo ya muto Yordani, ni kusema Sihoni na Ogi, ambao muliwaangamiza kabisa.
Halafu wazee wetu na wanainchi wote wa inchi yetu, wakatuambia, tutayarishe posho ya safari, tukuje kukutana nanyi na kuwaambia kwamba sisi ni watumishi wenu. Tafazali mufanye agano nasi.
Wakamujibu: “Sisi, watumishi wako, tumetoka inchi ya mbali na tumekuja kwa maana tumesikia sifa za jina la Yawe, Mungu wenu. Tulipata habari za utukufu wake na yote aliyoyafanya katika inchi ya Misri.