Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 8:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mukisha kuteka muji mutauteketeza kwa moto, kama vile Yawe alivyoamuru. Hayo ndiyo maagizo mutakayofuata.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 8:8
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abusaloma akawaambia watumishi wake: “Mumwangalie Amunoni atakapokuwa amekunywa divai na kufurahi. Nitakapowaambia: ‘Mumupige Amunoni’, mumwue. Hiyo ni amri yangu kwenu. Mujipe moyo na mukuwe hodari.”


Lakini katika miji ya inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa, musiache kitu chochote.


Wakamujibu Yoshua: “Mambo yote uliyotuamuru tutayafanya, na popote utakapotutuma tutakwenda.


Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”


Kisha, wakauchoma kwa moto muji wa Yeriko na kila kitu kilichokuwa mule isipokuwa feza, zahabu, vyombo vya shaba na vya chuma; hivyo viliwekwa katika hazina ya nyumba ya Yawe.


Kundi kubwa liliwekwa upande wa kaskazini wa muji na wale waliobaki waliwekwa upande wa magaribi wa muji. Lakini usiku ule, Yoshua akalala katika bonde.


Mutautendea muji wa Ai pamoja na mufalme wake kama vile mulivyoutendea muji wa Yeriko pamoja na mufalme wake. Mali zake pamoja na nyama wake mutakayoteka itakuwa ni mali yenu. Muende muushambulie muji kutoka upande wa nyuma.”


Watu waliobaki katika muji walitoka, lakini wote wakakuwa wamezungukwa na Waisraeli; nao wakauawa, wala hakukubaki hata mumoja wao.


Basi, Yoshua aliuteketeza muji wa Ai kwa moto na kuufanya mabomoko mpaka hivi leo.


Hapo, ninyi mutatokea kutoka kule mulikokuwa munavizia na kuuteka muji, maana Yawe, Mungu wenu, atautia muji huo katika mikono yenu.


Basi, Yoshua akawaambia waende pahali pao pa kuvizia; nao wakajiweka upande wa magaribi wa muji wa Ai, kati ya muji wa Ai na Beteli. Lakini Yoshua akalala usiku huo katika kambi ya Waisraeli.


Siku moja akamwita Baraka mwana wa Abinoamu wa Kedesi katika inchi ya Nafutali. Alipokuja akamwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli, anakuamuru hivi: ‘Kwenda ukusanye watu wako kwenye mulima Tabori, uchague watu elfu kumi kutoka makabila ya Nafutali na Zebuluni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ