Yoshua 8:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
6 Nao wataendelea kutufuatilia mpaka wakuwe mbali na muji wao, maana watafikiri kwamba wanatukimbiza kama vile walivyofanya mbele. Sisi tutawaacha watufukuze.
Mutu hajui saa yake itafika wakati gani. Kama vile samaki wanavyonaswa katika wavu kwa bahati mbaya, na kama vile ndege wanavyonaswa katika mutego kwa rafla, ndivyo wanadamu wanavyonaswa na hasara inapowaangukia bila kutazamia.
Watu wa Benjamina wakafikiri: “Tumewapiga kama nyakati zilizopita.” Lakini Waisraeli wakasema: “Sisi tukimbie kusudi tuwavute mbali na muji mpaka kwenye njia kubwa.”