Ingawa kulikuwa bado giza, mufalme aliamuka na kuwaambia wakubwa wa waaskari wake: “Mimi ninajua mupango wa Waaramu! Wanajua tuna njaa katika muji. Sasa wameacha kambi yao kwenda kujificha kusudi tutakapokwenda kutafuta chakula, watukamate wote tungali wazima na kuuteka muji.”
Lakini wakati ule, Yeroboamu alikuwa amekwisha kutuma waaskari wake wamoja kushambulia jeshi la Yuda kutoka upande wa nyuma, wakati wale wengine wamewashambulia kutoka upande wa mbele.
Lakini wewe usikubali ombi lao, kwa sababu kuna watu zaidi ya makumi ine wanaovizia kumwua. Watu hawa wamefanya kiapo kwamba hawatakula wala kunywa mpaka wamwue Paulo kwanza.”
Hivyo watu wote wa Israeli wakatoka kwenye sehemu yao na kujipanga tena kule Bali-Tamari. Wenzao waliokuwa wanafichama wakatoka haraka pahali pao upande wa magaribi wa muji wa Gibea.
Kwa hiyo watu wa kabila la Benjamina wakaona kwamba wameshindwa. Waisraeli wakarudi nyuma sawa vile wanawakimbia watu wa kabila la Benjamina, maana walitegemea wenzao waliokuwa wamewekwa kufichamia muji wa Gibea.
Watu wa Sekemu waliweka washambulizi wamuvizie Abimeleki kutoka vilele vya mulima. Watu hao waliwanyanganya mali zao wote waliopita kule. Abimeleki alipata habari hii.