Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 8:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Hakuna neno lililoamriwa na Musa ambalo Yoshua hakulisoma mbele ya Waisraeli, kati yao kukiwa wanawake, watoto na wageni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 8:35
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama naye akilia na kujiangusha uso mpaka chini mbele ya nyumba ya Mungu, kundi kubwa la watu wa Israeli, wanaume, wanawake na watoto, wakakusanyika karibu naye wakilia kwa uchungu mwingi.


Ezra, ambaye alikuwa kuhani, akaenda na kuleta kitabu cha Sheria ya Musa mbele ya mukutano wote, wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa ile sheria. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya kwanza ya mwezi wa saba.


Kisha Ezra akawasomea watu wote wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa Sheria ya Musa akiwa mbele ya Mulango wa Maji tangu asubui mpaka saa sita za muchana. Watu wote wakatega masikio yao na kusikiliza kwa uangalifu kitabu cha Sheria.


Kulikuwa vilevile kundi la watu wengine waliokwenda pamoja nao na mifugo mingi, kondoo na ngombe.


Yawe anasema hivi: Simama katika kiwanja cha nyumba ya Yawe, uwatangazie watu wa miji yote ya Yuda wanaofika kuabudu katika nyumba ya Mungu, mambo yote niliyokuamuru kuwaambia, bila kuacha hata neno moja.


Muwakusanye watu wote, muwatakase watu. Muwalete wazee, muwakusanye watoto, hata watoto wanaonyonya. Bwana-arusi na bibi-arusi watoke katika vyumba vyao.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Wakati ule, watu kumi kutoka mataifa ya kila luga watamukamatilia Muyuda mumoja na kushika nguo yake na kumwambia: Tunataka kwenda pamoja nanyi, kwa sababu tumesikia kwamba Mungu yuko pamoja nanyi.


Yesu alipoona vile, akakasirika na kuwaambia wanafunzi wake: “Muwaache watoto wadogo wakuje kwangu wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.


Ni vile kwa sababu niliwatangazia mupango wote wa Mungu pasipo kuwaficha kitu.


Lakini muda ule ulipotimia tukaondoka na kuendelea na safari yetu. Waamini wote pamoja na wanawake na watoto wao wakatusindikiza mpaka mbali na hata kufika kwenye kivuko cha muji. Kule sisi wote tukapiga magoti na kuomba.


watoto wenu na wake zenu, wageni wanaoishi kati yenu ambao wanakata kuni na kuwatekea maji.


Muko hapa leo kwa kufanya agano pamoja na Yawe, Mungu wenu na kulihakikisha kwa kiapo.


“Leo, mumesimama mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi wote viongozi wa makabila, wazee wenu, wakubwa wenu,


Mutakusanya wanaume, wanawake, watoto na wageni wanaoishi katika miji yenu, kusudi kila mumoja asikie maneno haya ya kujifunza kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kuwa waangalifu kushika maneno ya sheria hii.


Musiongeze chochote katika amri ninazowapa, wala musipunguze kitu. Mushike amri za Yawe, Mungu wenu, ambazo ninawapa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ