Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 8:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 kama vile Musa mutumishi wa Yawe alivyowaagiza Waisraeli, kadiri ilivyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa kwamba itakuwa mazabahu iliyojengwa kwa mawe ambayo hayakuchongwa, wala kuguswa na chombo chochote cha chuma. Juu ya mazabahu hiyo wakamutolea Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 8:31
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini hakuwaua watoto wa wauaji kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa, Yawe alipotoa amri akisema: “Wazazi hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya wazazi wao; lakini kila mutu atauawa kwa ajili ya zambi zake mwenyewe.”


Kisha Kuhani Mukubwa Hilkia akamwambia Safanu, mwandishi: “Nimekipata kitabu cha Sheria katika nyumba ya Yawe.” Halafu Hilkia akamupatia Safanu kitabu, naye akakisoma.


Lakini hakuwaua watoto wao, kama vile ilivyoandikwa katika sheria zinazokuwa katika kitabu cha Musa, ambamo Yawe anatoa amri akisema: “Wazazi hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya wazazi wao; lakini kila mutu atauawa kwa ajili ya zambi zake mwenyewe.”


Halafu wakatenga sadaka za kuteketeza kwa moto kusudi wapate kuzigawanya kwa watu kulingana na jamaa zao kusudi wamutolee Yawe kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Musa. Nao wakafanya vile vile na wale ngombe dume.


Vilevile, kwa ajili ya kazi ya Mungu katika Yerusalema, waliwapanga makuhani katika makundi yao ya Walawi katika zamu zao kufuatana na maagizo yaliyoandikiwa katika kitabu cha Musa.


Katika siku ile ya sherehe, kitabu cha Musa kikasomwa na ikajulikana kwamba Waamoni na Wamoabu hawaruhusiwi kuingia katika mukutano wa watu wa Mungu.


Halafu Yetro, baba mukwe wa Musa, akamutolea Mungu sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Naye Haruni akakuja pamoja na wazee wa Israeli kwa kula chakula pamoja na Yetro, mbele ya Yawe.


Kisha akatuma vijana wa watu wa Israeli wamutolee Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na kumuchinjia sadaka za amani za ngombe.


Na kama Shetani akimufukuza Shetani anajigombanisha yeye mwenyewe, nao ufalme wake utaanguka.


Siku ile mutakapovuka muto Yordani na kuingia katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, amewapa, mutasimika mawe makubwa na kuyapiga lipu.


Mutaandika waziwazi juu ya mawe hayo maneno yote ya sheria hii.”


Hakikisha kwamba hautakisahau hata kidogo kitabu hiki cha sheria; lakini kila siku utajifunza kitabu hiki, muchana na usiku, kusudi upate kutimiza yote yaliyoandikwa humu, nawe utastawi na kufanikiwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ