Yoshua 8:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
24 Waisraeli walipomaliza kabisa kuwaua watu wote wa Ai kule katika jangwa ambako waliwafuatilia wakarudi katika muji wa Ai na kuwaua wote waliobaki mule.
Lakini Waisraeli wakamwua kwa makali ya upanga, wakatwaa inchi yake, tangu muto Arnoni mpaka muto Yaboki, mpaka inchi ya Waamoni; nao mupaka wa inchi ya Amoni ulikuwa unalindwa sana.
Wakawakimbia Waisraeli kuelekea katika jangwa, lakini vita ikawapata. Wakajikuta wako katikati ya majeshi mawili ya Israeli, na waaskari waliotoka wakawaangamiza.