Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 8:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mutautendea muji wa Ai pamoja na mufalme wake kama vile mulivyoutendea muji wa Yeriko pamoja na mufalme wake. Mali zake pamoja na nyama wake mutakayoteka itakuwa ni mali yenu. Muende muushambulie muji kutoka upande wa nyuma.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 8:2
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wakati ule, Yeroboamu alikuwa amekwisha kutuma waaskari wake wamoja kushambulia jeshi la Yuda kutoka upande wa nyuma, wakati wale wengine wamewashambulia kutoka upande wa mbele.


Wakati walipoanza kuimba na kusifu, Yawe akawavuruga akili waaskari Waamoni, Wamoabu na watu wa mulima Seiri waliokuja kupigana na Yuda. Na waaskari wale wakashindwa.


Kumbe umenipimia maisha mafupi sana! Maisha yangu si kitu mbele yako. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.


Mutu mwaminifu atapata baraka tele, lakini mwenye pupa ya kuwa tajiri hataepuka azabu.


Mutu anayepata mali isiyokuwa ya usawa ni kama kwale anayelalia mayai ambayo hakutaga. Mali yanamwishia angali kijana, na kwa mwisho anageuka sawa mupumbafu.


Mupandishe bendera ya vita kwa kushambulia kuta za Babeli. Muimarishe walinzi, muweke walinzi, mutayarishe mashambulizi. Yawe amepanga na kutimiza mambo aliyosema juu ya wakaaji wa Babeli.


Tulibeba tu mifugo na mali tuliyokuta katika miji tuli Yosinda.


Lakini wanawake na watoto, ngombe, na vyote vinavyokuwa katika muji, vitu vyake vyote munaweza kuvibeba kwa ajili yenu wenyewe. Munaweza kufurahia vitu vya waadui zenu, ambavyo Yawe, Mungu wenu, amewapa.


Lakini Yawe akaniambia: ‘Usimwogope, maana nimemutia katika mikono yako pamoja na watu wake na inchi yake. Utamutendea kama vile ulivyomutendea Sihoni mufalme wa Waamori aliyekaa kule Hesiboni’.


Mufalme Adoni-Zedeki wa Yerusalema akapata habari juu ya jinsi Yoshua alivyouteka muji wa Ai na kuuharibu kabisa akiutendea muji huo na mufalme wake kama alivyoutendea Yeriko na mufalme wake. Vilevile akapata habari kwamba wakaaji wa Gibeoni walikuwa wamefanya mapatano ya amani na Waisraeli na kwamba sasa wanaishi kati yao.


Siku hiyo Yoshua alipouteka muji wa Makeda, alimuua mufalme wake na wakaaji wake wote bila kuacha hata mutu mumoja. Alimutendea mufalme wa Makeda kama vile alivyomutendea mufalme wa Yeriko.


Waisraeli wakatwaa vitu vyote walivyonyanganya na nyama wa miji hiyo; lakini waliwaua wakaaji wake wote, wala hawakumwacha hata mutu mumoja.


Kisha wakaangamiza kila kitu katika muji ule na kuwaua kwa upanga: wanaume na wanawake, vijana na wazee, ngombe, kondoo na punda.


Halafu akatwaa watu wengine elfu tano na kuwaweka wavizie kati ya muji wa Beteli na Ai, upande wa magaribi wa muji wa Ai.


Mufalme wa muji wa Ai alipoona hivyo, alifanya haraka na kwenda kwenye muteremuko wa kuelekea Araba kwa kushambulia Waisraeli katika vita. Lakini hakujua kwamba muji wake ulikuwa umeviziwa kutoka nyuma.


Mara tu Yoshua alipouelekeza mukuki wake kule Ai, kundi lililokuwa likivizia upande mwingine likatoka na kuingia katika muji. Likauteka muji na kuuteketeza kwa moto.


Waisraeli walipomaliza kabisa kuwaua watu wote wa Ai kule katika jangwa ambako waliwafuatilia wakarudi katika muji wa Ai na kuwaua wote waliobaki mule.


Basi, Yoshua akaondoka, pamoja na waaskari wake wote kwenda Ai. Akawachagua watu hodari elfu makumi tatu na kuwaambia watangulie wakati wa usiku.


Hapo, ninyi mutatokea kutoka kule mulikokuwa munavizia na kuuteka muji, maana Yawe, Mungu wenu, atautia muji huo katika mikono yenu.


Mukisha kuteka muji mutauteketeza kwa moto, kama vile Yawe alivyoamuru. Hayo ndiyo maagizo mutakayofuata.”


Basi, Yoshua akawaambia waende pahali pao pa kuvizia; nao wakajiweka upande wa magaribi wa muji wa Ai, kati ya muji wa Ai na Beteli. Lakini Yoshua akalala usiku huo katika kambi ya Waisraeli.


Lakini wakaaji wa Gibeoni walipopata habari juu ya jinsi Yoshua alivyoitendea miji ya Yeriko na Ai,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ