Yoshua 8:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
19 Mara tu Yoshua alipouelekeza mukuki wake kule Ai, kundi lililokuwa likivizia upande mwingine likatoka na kuingia katika muji. Likauteka muji na kuuteketeza kwa moto.
Halafu Yawe akamwambia Yoshua: “Elekeza mukuki wako kule katika muji wa Ai maana nitautia muji ule katika mikono yako.” Yoshua akaelekeza mukuki wake kwenye muji wa Ai.
Mutautendea muji wa Ai pamoja na mufalme wake kama vile mulivyoutendea muji wa Yeriko pamoja na mufalme wake. Mali zake pamoja na nyama wake mutakayoteka itakuwa ni mali yenu. Muende muushambulie muji kutoka upande wa nyuma.”
Watu wa Ai walipoangalia nyuma, wakaona moshi ukitoka katika muji ukipanda mpaka mbinguni. Nao hawakukuwa na uwezo wa kukimbia upande wowote, maana Waisraeli waliwageukia wale waliokuwa wanawafuatilia.
Hivyo watu wote wa Israeli wakatoka kwenye sehemu yao na kujipanga tena kule Bali-Tamari. Wenzao waliokuwa wanafichama wakatoka haraka pahali pao upande wa magaribi wa muji wa Gibea.