Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 8:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Hakuna mutu yeyote aliyebaki katika muji wa Ai, waliuacha muji ule wazi wakaenda kuwafuatilia Waisraeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 8:17
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anawanasa wenye hekima kwa werevu wao, anakomesha mara moja mipango ya waovu.


“Lakini Sihoni, mufalme wa Hesiboni, hakuturuhusu tupite katika inchi yake. Yawe, Mungu wenu, akamufanya akuwe na kichwa kigumu na mugumu wa moyo, kusudi tumushinde na kutwaa inchi yake ambayo tunairizi mpaka leo.


Ilikuwa ni mapenzi ya Yawe mwenyewe kuifanya mioyo ya watu wa mataifa hayo kuwa migumu kusudi wapigane. Alikusudia wasihurumiwe lakini wateketezwe. Ndivyo Yawe alivyomwamuru Musa.


Watu wote waliokuwa katika muji wakaitwa wawafuatilie Waisraeli; na walipokuwa wanamufuatilia Yoshua, walitoka na kwenda mbali na muji wao.


Halafu Yawe akamwambia Yoshua: “Elekeza mukuki wako kule katika muji wa Ai maana nitautia muji ule katika mikono yako.” Yoshua akaelekeza mukuki wake kwenye muji wa Ai.


Basi, Yoshua akaondoka, pamoja na waaskari wake wote kwenda Ai. Akawachagua watu hodari elfu makumi tatu na kuwaambia watangulie wakati wa usiku.


Kisha watu wa kabila la Benjamina walipotoka katika muji kwa kuanza kupigana na Waisraeli, walivutwa kutoka inje ya muji. Ilitokea tena kama walivyofanya nyakati za mbele. Wakawaua wamoja kati ya watu wa Israeli kwenye njia kubwa zinazoelekea miji ya Beteli na Gibea, mpaka katika mbuga. Waliua Waisraeli yapata makumi tatu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ