Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 8:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Mufalme wa muji wa Ai alipoona hivyo, alifanya haraka na kwenda kwenye muteremuko wa kuelekea Araba kwa kushambulia Waisraeli katika vita. Lakini hakujua kwamba muji wake ulikuwa umeviziwa kutoka nyuma.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 8:14
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutu hajui saa yake itafika wakati gani. Kama vile samaki wanavyonaswa katika wavu kwa bahati mbaya, na kama vile ndege wanavyonaswa katika mutego kwa rafla, ndivyo wanadamu wanavyonaswa na hasara inapowaangukia bila kutazamia.


Wakubwa wa muji wa Soani ni wapumbafu kabisa, washauri wa Mufalme wa Misri wanatoa shauri la kijinga! Kila mumoja anaweza namna gani kumwambia Mufalme wa Misri: Mimi ni wa uzao wa wenye hekima, wa uzao wa wafalme wa zamani!


Lakini wakubwa wa Soani ni wapumbafu, wakubwa wa Nofi wamedanganyika. Hao wanaokuwa musingi wa makabila yao wamelipotosha taifa la Misri.


Kwa mwisho wa ile miaka saba, mimi Nebukadneza niliinua macho yangu kuangalia juu mbinguni na akili zangu zikanirudilia. Nilimushukuru Mungu Mukubwa na kumuheshimu yeye anayeishi milele: Kwa sababu mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ufalme wake unadumu kwa vizazi vyote.


Nao hawakutambua kitu mpaka mvua kubwa sana ilipotokea, na kuwaua wote. Na ni hivi itakavyokuwa wakati Mwana wa Mutu atakaporudi.


Basi bwana wa mutumishi yule atakuja siku asiyozania na saa asiyojua.


Kitabu hiki kina maneno ambayo Musa aliwaambia watu wote wa Israeli wakati walipokuwa katika jangwa upande wa mashariki wa muto Yordani. Walikuwa katika bonde la Yordani karibu na Sufu, kati ya muji wa Parani upande mumoja na miji ya Tofeli, Labani, Hazeroti na Dizahabu upande mwingine.


Kundi kubwa liliwekwa upande wa kaskazini wa muji na wale waliobaki waliwekwa upande wa magaribi wa muji. Lakini usiku ule, Yoshua akalala katika bonde.


Kisha Yoshua pamoja na watu wake wakajifanya sawa wenye kushindwa, wakaanza kukimbia kuelekea katika jangwa.


Watu wote waliokuwa katika muji wakaitwa wawafuatilie Waisraeli; na walipokuwa wanamufuatilia Yoshua, walitoka na kwenda mbali na muji wao.


Mimi, pamoja na watu wote wanaokuwa pamoja nami, tutaukaribia muji. Watakapotoka inje kuja kutushambulia kama pale mbele, sisi tutawakimbia.


Na kwa sababu ya tamaa yao mbaya ya mali, walimu hawa wa uongo watajipatia faida juu yenu kwa njia ya maneno ya uongo. Lakini tangia zamani hukumu yao imekwisha kutangazwa, nao hawatakawia kuangamizwa.


Wale waliowekwa kufichamia muji walitoka haraka na kuushambulia muji wa Gibea na kuwaua wote waliokuwa mule kwa upanga.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ