Mimi nitasimama pahali pa kuchungulia, na kuikaa juu katika munara; nitakaa macho wazi nipate kuona ataniambia nini, atajibu nini juu ya malalamiko yangu.
Yoshua akasema: “Ole wetu, ee Bwana wetu Yawe! Kwa nini umetuvukisha muto Yordani kwa kututia katika mikono ya Waamori kusudi watuangamize? Tungalifurahi kubaki ngambo ya muto Yordani!
Basi, Wakanana pamoja na wakaaji wote wa inchi hii watakapopata habari hiyo watatuzunguka na kutufuta kabisa katika dunia. Sasa utafanya nini kwa kuonyesha ukubwa wa jina lako?”
Waaskari walioponyoka walipofika kwenye kambi, wazee wa Israeli walisema: “Kwa nini Yawe amewaacha Wafilistini watushinde leo? Tuende tulilete Sanduku la Agano la Yawe kutoka Shilo, kusudi aweze kwenda nasi katika vita na kutuokoa kutoka waadui zetu.”