Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 7:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Yoshua akamwuliza Akana: “Kwa nini umetuletea taabu? Yawe atakuletea taabu wewe mwenyewe leo.” Waisraeli wote wakamupiga Akana kwa mawe mpaka akakufa. Kisha wakawapiga jamaa yake yote kwa mawe mpaka wakakufa, wakawateketeza wote kwa moto.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 7:25
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yakobo akamwambia Simeoni na Lawi: “Ninyi mumeniletea taabu kwa kunifanya nichukiwe na wakaaji wa inchi hii ya Wakanana na Waperizi. Mimi sina watu wengi, na kama wakikusanyika kwa kunishambulia wataniangamiza mimi pamoja na jamaa yangu.”


Kisha miezi mitatu, Yuda akapata habari hii: “Tamari, muke wa mwana wako amekuwa kahaba, tena amepata mimba kwa kufanya ukahaba.” Basi, Yuda akaamuru: “Mumutoshe inje achomwe kwa moto!”


Mwana wa Karmi alikuwa: Akana, ni kusema “Taabu”. Huyu aliwaletea Waisraeli taabu kwa sababu alijiwekea vitu vilivyolaaniwa.


Ndizo njia za wanyanganyi; maisha yao yananyanganywa.


Anayetamani faida ya unyanganyi anataabisha jamaa yake, lakini anayechukia kituliro ataishi.


Kama mwanaume akioa muke na vilevile kumwoa mama yake, huo ni uovu. Wote watatu wanapaswa kuteketezwa kwa moto maana wamefanya uovu. Mutafanya hivyo kwa kukomesha uovu kati yenu.


Uwaambie Waisraeli hivi: Mutu yeyote kati ya Waisraeli au mugeni anayekaa kati yenu, akimutoa mutoto wake yeyote kuwa sadaka kwa mungu Moleki, mutu huyu anapaswa kuuawa. Wanainchi wa pale watamwua kwa kumupiga mawe.


Binti wa kuhani yeyote akijichafua kwa kufanya ukahaba, atateketezwa kwa moto maana anamuchafua baba yake.


Umuondoe kijana aliyetukana inje ya kambi, wale wote waliomusikia akitukana waweke mikono yao juu ya kichwa chake, na wote pamoja wamwue kwa kumupiga mawe.


Heri wale wanaoleta fujo kati yenu wangejikata viungo vyao vya uzazi.


lakini utamwua. Mukono wako unapaswa ukuwe wa kwanza wakati wa kumwua halafu wengine wote watafuata vilevile.


Umupige mawe mpaka akufe, kwa sababu amejaribu kukuvuta mbali kutoka kwa Yawe, Mungu wako, ambaye alikutoa toka utumwa katika inchi ya Misri.


basi, mumupeleke mutu huyo inje ya miji na kumupiga mawe mpaka akufe.


Hapo watu wa muji huo watamupiga mutoto huyo mawe mpaka akufe. Ndivyo mutakavyokomesha ubaya huo kati yenu. Kila mutu katika Israeli atasikia tukio hilo na kuogopa.


Kwa maana, Mungu yuko na haki ya kuwatesa wale wanaowatesa ninyi,


Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi.


Lakini musitwae kitu chochote ambacho kimetolewa kusudi kiangamizwe. Mukitwaa kitu chochote ambacho kimetolewa kusudi kiangamizwe, mutaifanya kambi ya Israeli kuwa kitu cha kuangamizwa, na hivyo kuiletea hasara.


Mutu yeyote atakayepatikana akiwa na vitu vilivyotolewa viangamizwe atateketezwa kwa moto, yeye pamoja na kila kitu chake maana ameliasi agano langu mimi Yawe, akatenda jambo la haya katika Israeli.’ ”


Yonatani akajibu: “Baba yangu anawasumbua watu. Sasa mimi ninajisikia kuwa na nguvu kwa sababu nimeonja asali hii kidogo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ