Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 7:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Nilipoona vazi moja zuri kutoka Sinari kati ya vitu tulivyonyanganya, vikoroti mia mbili vya feza na furushi ya zahabu yenye uzito wa vikoroti makumi tano vya feza, nikavitamani na kuvitwaa; nikavificha katika udongo ndani ya hema langu; na feza iko chini ya vitu hivyo.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 7:21
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Miji ya kwanza ya utawala wake ilikuwa Babeli, Ereki, na Akadi katika inchi ya Sinari.


Basi, mwanamuke alipoona kwamba muti ule ni muzuri kwa chakula, unavutia macho, na kwamba unafaa kwa kupata hekima, akachuma tunda lake, akakula, akamupa mume wake aliyekuwa pamoja naye, naye vilevile akakula.


Nyuma ya mauaji hayo, wana wengine wa Yakobo wakaingia katika muji na kunyanganya mali yote katika muji ule, kwa sababu dada yao alikuwa amechafuliwa.


wana wa Mungu wakaona kwamba wale wabinti za watu ni wazuri, wakawatwaa wale waliowapendeza kuwa wake zao.


Siku moja, wakati wa magaribi, Daudi aliamuka toka katika kitanda, akaenda kwenye dari ya nyumba ya kifalme. Alipokuwa anatembea kule juu, alimwona mwanamuke mumoja akioga na mwanamuke yule alikuwa muzuri sana kwa umbo.


Wale watu wane wenye ukoma walipofika pembeni ya kambi, waliingia ndani ya hema moja, wakakula na kunywa vile walivyopata mule, wakatwaa feza, zahabu na nguo, wakaenda kuzificha. Wakaingia katika hema ingine na kufanya vivyo hivyo.


Nimejizuiza kabisa mimi mwenyewe, macho yangu yasimwangalie binti kwa tamaa.


Uniepushe nisifuate mambo ya ovyo; unionyeshe njia yako, unipe uzima.


Usitamani nyumba ya mwenzako, wala muke wake, wala mutumwa wake au mujakazi wake, wala ngombe wake, wala punda wake, wala kitu chochote mwenzako anachokuwa nacho.


Ndizo njia za wanyanganyi; maisha yao yananyanganywa.


Usiitamani divai hata kwa wekundu wake, hata kama inametameta katika kilauri, na kushuka vizuri unapoikunywa.


Mutu muchoyo anakimbilia mali, wala hajui kwamba ukosefu utamufikia.


Linda moyo wako kwa uangalifu wote, maana mule munatokea chemichemi za uzima.


Ninyi munajidai mumefanya agano na kifo mumefanya mapatano na kuzimu! Ninyi munasema kwamba hasara itakapokuja haitawapata, kwa sababu mumefanya uongo kuwa tegemeo lenu, na udanganyifu kuwa kikingio chenu!


Ole kwenu ninyi munaomuficha Yawe mipango yenu, munaotenda matendo yenu katika giza na kusema: Hakuna atakayetuona; nani anayeweza kujua tunachofanya?


Ole wako unayejitajirisha kwa hasara ya mwingine, unayejenga nyumba yako juu katika milima ukizani kuwa salama mbali na hasara.


Kisha Yesu akawaambia watu wote: “Muangalie, mujilinde na tamaa yote ya mali, kwa sababu mali haiwezi kukinga uzima wa mutu, hata akiwa tajiri sana.”


Hakuna kitu chochote kinachofichwa kitakachokosa kuvumbulikana wala hakuna siri itakayokosa kujulikana.


Kama vile inavyowapasa watu wa Mungu kuishi, tendo lolote la uasherati, la uchafu wala la tamaa ya mali lisisikilike kati yenu.


Mujue waziwazi kwamba mwasherati yeyote na muchafu na mwenye tamaa ya mali (mwenye tamaa ni kama mwenye kuabudu sanamu), hao wote hawatapewa sehemu ya urizi katika Ufalme wa Kristo na Mungu.


Muteketeze kwa moto sanamu za miungu yao. Musitamani feza wala zahabu yao, wala musiitwae na kuifanya mali yenu. Kufanya hivyo ni mutego kwenu na ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu.


Basi mutupilie mbali mambo yote ya kidunia yanayokuwa ndani yenu: uasherati, uchafu, nia mbaya, tamaa mbaya na tamaa ya mali inayokuwa sawa vile kuabudu sanamu.


Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”


Halafu ile tamaa mbaya ikisha kukomaa, inazaa zambi, nayo zambi ikisha kukomaa inazaa lufu.


Akana akamujibu: “Ni kweli nimetenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wa Israeli. Na hivi ndivyo nilivyofanya:


Basi, Yoshua akawatuma wajumbe, nao wakakimbia kwenye hema kwa Akana. Na kumbe, vitu vilikuwa vimefichwa katika hema na feza ikiwa chini yake.


Wameacha njia ya kweli na kupotoka wakifuata njia ile Balama, mwana wa Beori, aliyofuata. Huyu alipenda kupata mali kwa njia isiyokuwa ya haki,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ