Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yoshua akawatuma watu kutoka Yeriko kwenda muji wa Ai, unaokuwa karibu ya Beti-Aweni, upande wa mashariki wa Beteli, akawaambia: “Mwende muipeleleze inchi.” Nao wakaenda na kuupeleleza muji wa Ai.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 7:2
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Abramu akaondoka, akaelekea kwenye mulima upande wa mashariki ya Beteli akapiga hema kati ya muji wa Beteli, upande wa magaribi, na muji wa Ai upande wa mashariki. Pale vilevile akamujengea Yawe mazabahu na kumwomba kwa jina lake.


Akaita pahali hapo Beteli, ni kusema “Nyumba ya Mungu”. Jina la mbele la muji ule lilikuwa Luzi.


Akaiweka sanamu moja katika muji wa Beteli, na ya pili katika muji wa Dani.


Watu wa kabila la Benjamina walikaa Geba, Mikimasi, Ai, Beteli na vijiji vinavyoizunguka.


Mipango mizuri inafanyika kwa kushauriana; ukitaka kuanza vita inafaa kufikiri kwanza.


Maana kwa mipango mizuri unaweza kupigana vita, na kwa washauri wengi ushindi unapatikana.


amefika katika muji wa Ayati. Amepitia kule Migoroni, mizigo yake ameiacha katika muji wa Mikimasi.


Muomboleze, enyi watu wa Hesiboni, maana muji Ai umeharibika! Mulie, enyi wabinti wa Raba! Muvae magunia, muomboleze na kukimbia huko na huko ndani ya ukuta wenu! Maana mungu Milkomu atapelekwa katika uhamisho, pamoja na makuhani wake na watumishi wake.


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


“Muangalie! Ninawatuma kama kondoo katikati ya imbwa wa pori. Basi mukuwe waangalifu kama nyoka na wakamilifu kama njiwa.


Muangalie vizuri mwenendo wenu. Musiishi kama wajinga lakini muishi kama wenye hekima.


Wafalme walioshindwa walikuwa, mumoja kwa mwengine: mufalme wa Yeriko, mufalme wa Ai muji unaokuwa karibu na Beteli,


Mupaka wake wa kaskazini ulianzia kwenye muto Yordani na kupitia upande wa kaskazini wa Yeriko na inchi ya milima ukaelekea upande wa magaribi mpaka kwenye jangwa la Beti-Aweni.


Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kwa siri kutoka Sitimu waende kufanya upelelezi katika inchi ile na hasa muji wa Yeriko. Wakaenda, wakafika kwenye nyumba ya kahaba mumoja aliyeitwa Rahabu wakalala humo.


Waliporudi, wakamwambia Yoshua: “Hakuna lazima ya kupeleka watu wote kuushambulia muji wa Ai, maana wakaaji wake ni wachache tu. Watu elfu mbili au tatu watatosha.”


Wafilistini walikuwa na magari elfu makumi tatu, waaskari elfu sita wapanda-farasi na kikundi cha waaskari wa miguu wengi kama muchanga wa bahari. Wote walipanda juu na kupiga kambi yao kule Mikimasi, upande wa mashariki wa Beti-Aweni.


Hivyo Yawe aliwapa Waisraeli ushindi. Vita ilienea mpaka kupita Beti-Aweni.


Zawadi hizo zilikuwa kwa ajili ya wakaaji wa Beteli, wakaaji wa Ramoti katika Negebu, wakaaji wa Yatiri,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ