Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 7:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kwa hiyo Waisraeli hawawezi kuwashinda waadui zao. Wanawakimbia waadui zao kwa sababu wamejifanya wenyewe kuwa kitu cha kuangamizwa! Sitakuwa pamoja nao tena musipoharibu vitu vinavyokuwa kati yenu vilivyotolewa viangamizwe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 7:12
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini sasa umetuacha na kutufezehesha; hauendi tena na makundi yetu ya waaskari.


Moabu ni kama bakuli langu la kunawia. Nitatupia Edomu kiatu changu kwa kuirizi. Nitapiga kelele la ushindi juu ya Filistia.”


Waovu wanakimbia ijapokuwa hawafukuzwi na mutu, lakini wenye haki ni hodari kama simba.


Zambi zenu ndizo zinazowatenga na Mungu wenu, zambi zenu zimemufanya ajifiche mbali nanyi hata asiweze kuwasikiliza ninyi.


Yawe akaniambia: Mutu yeyote, akuwe nabii au kuhani akikuuliza “Uko wapi muzigo Yawe anaotubebesha?”, wewe utawaambia: Ninyi ndio muzigo kwa Yawe, naye atawatupa mbali. –Ni ujumbe wa Yawe!–


Basi usikilize maonyo, ee Yerusalema. Kama sivyo nitakutupilia mbali; nitakufanya ukuwe jangwa, kuwa pahali pasipokaliwa na mutu.


Hata kama wakilea watoto, sitamwacha hata mumoja wao muzima. Ole kwao, nitakapowaacha peke yao!


Wewe ni mutakatifu kabisa, hauwezi kutazama uovu, hauwezi kuvumilia hata kidogo kuona mabaya. Mbona basi unawaona wafanya maovu na kunyamaza, kwa nini unanyamaza waovu wanapowamaliza wale watu wanaokuwa wenye haki kuliko wao?


Musa akawaambia Waisraeli wote nao wakalia kwa uchungu mwingi.


Musiende kule kwenye milima kusudi musipigwe bure na waadui zenu, maana, Yawe hayuko pamoja nanyi.


Mukiwashambulia Waamaleki na Wakanana, mutakufia katika vita kwa sababu mumeacha kumufuata Yawe. Yeye hatakuwa pamoja nanyi.


Halafu Waamaleki na Wakanana, waliokuwa wakiishi katika inchi hiyo ya milima, wakashuka, wakawashambulia na kuwashinda. Wakawafukuza mpaka muji wa Horma.


Musipeleke sanamu zozote katika nyumba zenu, kama sivyo, mutalaaniwa kama sanamu hizo. Muzichukie na kuzizarau kwa sababu ni vitu vilivyolaaniwa.


Lakini musitwae kitu chochote ambacho kimetolewa kusudi kiangamizwe. Mukitwaa kitu chochote ambacho kimetolewa kusudi kiangamizwe, mutaifanya kambi ya Israeli kuwa kitu cha kuangamizwa, na hivyo kuiletea hasara.


Delila akamwambia Samusoni: “Samusoni! Wafilistini wanakuja kukushambulia!” Samusoni akaamuka toka katika usingizi naye akifikiri kwamba atatoka na kujiokoa kama vile mbele. Kumbe hakujua kwamba Yawe alikuwa amemwacha.


Basi, hasira ya Yawe ikawaka juu ya Israeli, naye akawaacha wanyanganyi wanyanganye mali zao. Akawatoa kwa waadui zao waliowazunguka hata wasiweze tena kuwashinda.


Malaika wa Yawe alipowaambia watu wote wa Israeli maneno haya, wakalalamika na kulia.


Saulo akasema: “Mukuje hapa enyi viongozi wa watu, tujue ni zambi gani tumetenda leo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ