Wake zenu, watoto wenu na nyama wenu wa kufugwa watabaki katika inchi hiyo ambayo Musa aliwapa, ngambo ya muto Yordani. Lakini wanaume wote hodari wakiwa na silaha watavuka muto na kuwatangulia wandugu zenu.
Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawaita makuhani, akawaambia: “Mulibebe Sanduku la Agano na makuhani saba watwae mabaragumu saba ya kondoo dume, watangulie mbele ya Sanduku la Yawe.”
Kulingana na amri ya Yoshua, wale makuhani saba waliokuwa na mabaragumu saba ya kondoo dume wakaenda mbele ya Yawe, wakiwa wanapiga mabaragumu, nyuma yao wakifuatwa na lile Sanduku la Agano.