Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 6:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Basi, Yoshua mwana wa Nuni, akawaita makuhani, akawaambia: “Mulibebe Sanduku la Agano na makuhani saba watwae mabaragumu saba ya kondoo dume, watangulie mbele ya Sanduku la Yawe.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 6:6
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Miti ile utaipitisha katika pete zinazokuwa kwa pande mbili za sanduku, kwa ajili ya kulibeba.


Katika siku zile zile, Saulo aliendelea na vitisho vikali vya kuwaua wanafunzi wa Bwana. Siku moja akamwendea Kuhani Mukubwa


Halafu mukavuka muto Yordani, mukafika Yeriko. Wakaaji wa Yeriko walipigana nanyi, vilevile na Waamori, Waperizi, Wakanana, Wahiti, Wagirgasi, Wahivi na Wayebusi. Hao mimi nikawatia katika mikono yenu.


wakawaambia watu: “Mutakapoliona Sanduku la Agano la Yawe, Mungu wenu, limebebwa na makuhani Walawi, mutaondoka na kulifuata;


Kisha akawaambia makuhani: “Mutwae Sanduku la Agano, mutangulie nalo mbele ya watu.” Nao wakalitwaa na kutangulia mbele ya watu.


Wale makuhani saba wenye mabaragumu saba ya kondoo dume walitembea mbele ya Sanduku la Yawe wakipiga mabaragumu kwa mufululizo. Watu wenye silaha walilitangulia Sanduku la Yawe na walinzi wengine nyuma yake. Mabaragumu yakaendelea kupigwa.


Watakapopiga hayo mabaragumu kwa mulio mukubwa na mara tu mutakaposikia huo mulio, watu wote watapiga kelele kubwa, nazo kuta za muji zitaanguka chini. Halafu watu wataushambulia muji kila mumoja kutoka pahali aliposimama.”


Yoshua akawaambia watu: “Mupite mbele, muzunguke muji, nao watu wenye silaha waende mbele ya Sanduku la Agano la Yawe.”


Kulingana na amri ya Yoshua, wale makuhani saba waliokuwa na mabaragumu saba ya kondoo dume wakaenda mbele ya Yawe, wakiwa wanapiga mabaragumu, nyuma yao wakifuatwa na lile Sanduku la Agano.


Waaskari walioponyoka walipofika kwenye kambi, wazee wa Israeli walisema: “Kwa nini Yawe amewaacha Wafilistini watushinde leo? Tuende tulilete Sanduku la Agano la Yawe kutoka Shilo, kusudi aweze kwenda nasi katika vita na kutuokoa kutoka waadui zetu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ