Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 6:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Makuhani saba, kila mumoja akiwa anabeba baragumu yake ya pembe ya kondoo dume, watatangulia mbele ya Sanduku la Agano. Katika siku ya saba mutauzunguka muji ule mara saba, nao makuhani wakipiga mabaragumu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 6:4
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akaibariki siku ya saba na kuitakasa, maana kwa siku hiyo Mungu alipumzika kisha kazi yake yote ya kuumba.


Kisha akamwambia mutumishi wake: “Sasa, kwenda uangalie kwa upande wa bahari.” Mutumishi akaenda, akaangalia, kisha akarudia akasema: “Hakuna kitu.” Elia akamwambia: “Kwenda tena mara saba.”


Elisha akamutuma mutumishi wake amwambie: “Kwenda uoge mara saba katika muto Yordani, nawe utapona kabisa.”


Basi, Namani akateremuka kwenye muto Yordani akajitumbukiza mule mara saba, kama alivyoagizwa na Elisha mutu wa Mungu, naye akapona kabisa. Ngozi yake ikakuwa laini na yenye afya kama ya mutoto mudogo.


Na muangalie, Mungu mwenyewe ndiye kiongozi wetu na makuhani wake wako na baragumu zao tayari kuzipiga kwa kupana kitambulisho cha kuanza vita juu yenu. Enyi watu wa Israeli, muache kupigana vita na Yawe, Mungu wa babu zenu. Hamuwezi kushinda!”


Hamutahitaji kupigana vita hivi. Ninyi mujipange tu halafu mungojee, na mutaona Yawe akiwashinda kwa jina lenu. Enyi watu wa Yuda na Yerusalema, musiogope wala musifazaike. Muende kwa vita, naye Yawe atakuwa pamoja nanyi!”


Walawi na ukoo wa Kohati na Kora, wakasimama na kumusifu Yawe, Mungu wa Israeli, kwa sauti kubwa sana.


Nyuma ya kushauriana na watu, mufalme akachagua waimbaji kwa kumwimbia Yawe wavae nguo zao takatifu kisha watangulie mbele ya jeshi, wakiimba: “Mumushukuru Yawe, maana wema wake unadumu milele!”


Kwa hiyo mutwae ngombe dume saba na kondoo dume saba, muende kwa mutumishi wangu Yobu, mutoe nyama wale kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Naye mutumishi wangu Yobu atawaombea, nami nitaisikiliza maombi yake na kuacha kuwatendea kulingana na upumbafu wenu; maana hamukusema ukweli juu yangu kama mutumishi wangu Yobu alivyofanya.”


Siku hiyo, baragumu kubwa itapigwa na watu wote wa Israeli waliopotea katika inchi ya Asuria au waliotawanywa katika inchi ya Misri watarudi na kumwabudu Yawe juu ya mulima mutakatifu kule Yerusalema.


Atachovya kidole cha mukono wake wa kuume katika mafuta hayo na kumunyunyizia yule mutu anayetakaswa mara saba mbele ya Yawe.


Atachovya kidole chake katika damu hiyo na kuinyunyiza mara saba mbele ya Yawe upande wa mbele wa pazia la Pahali Patakatifu.


Akaniuliza: Unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kinara cha taa cha zahabu. Juu yake kuna bakuli la mafuta na taa saba, na kila moja ina pahali pa kutilia tambi saba.


Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.


Balamu akamwambia Balaki: Unijengee mazabahu saba hapa kisha uniletee ngombe dume saba na kondoo dume saba.


Wale makuhani saba wenye mabaragumu saba ya kondoo dume walitembea mbele ya Sanduku la Yawe wakipiga mabaragumu kwa mufululizo. Watu wenye silaha walilitangulia Sanduku la Yawe na walinzi wengine nyuma yake. Mabaragumu yakaendelea kupigwa.


Wewe na wale watu wenye silaha wote mutauzunguka ule muji mara moja kila siku kwa muda wa siku sita.


Watakapopiga hayo mabaragumu kwa mulio mukubwa na mara tu mutakaposikia huo mulio, watu wote watapiga kelele kubwa, nazo kuta za muji zitaanguka chini. Halafu watu wataushambulia muji kila mumoja kutoka pahali aliposimama.”


Hii ndiyo maana ya lile fumbo juu ya zile nyota saba ulizoona katika mukono wangu wa kuume, na vile vinara saba vya zahabu: zile nyota saba ni wamalaika wa makanisa saba na vile vinara saba ni yale makanisa saba.


Ni mimi Yoane ninayewaandikia ninyi makanisa saba munaokuwa katika jimbo la Azia. Ninawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja, na kutoka kwa roho saba wanaokuwa mbele ya kiti chake cha kifalme,


Akalalamika kwa sauti kubwa kama simba anayenguruma. Na alipokwisha kulalamika, kukasikilika mulio wa ngurumo saba ya radi.


Kisha nikaona tena katika mbingu kitambulisho kingine kikubwa na cha kushangaza sana. Kulikuwa wamalaika saba wanaoshika mapigo saba. Mapigo haya ndiyo yaliyokuwa ya mwisho, kwa maana ni yale Mungu atakayotumia kwa kutimiza kasirani yake.


Na mumoja wa vile viumbe vine vya ajabu akawapa wale wamalaika saba vikombe saba vya zahabu vyenye kujaa kasirani ya Mungu, anayeishi kwa milele.


Kisha nikasikia sauti kubwa ikitoka katika hekalu ikiwaambia wale wamalaika saba: “Mwende kumwanga vile vikombe saba vya kasirani ya Mungu juu ya dunia!”


Kisha nikaona kizingo cha karatasi katika mukono wa kuume wa yule aliyeikaa juu ya kiti cha kifalme. Kizingo kile kilikuwa kimeandikwa ngambo na ngambo na kufungwa kwa vifundo saba vya mihuri.


Halafu nikaona Mwana-Kondoo akisimama katikati ya kiti cha kifalme chenye kuzungukwa na vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee, naye alionekana kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba; ndizo roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote.


Kisha nikaona wamalaika saba wakisimama mbele ya Mungu, nao wakapewa baragumu saba.


Wale wamalaika saba waliokuwa na baragumu saba wakajitayarisha kwa kuzipiga.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ