Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 6:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Wakati ule Yoshua akaapa mbele ya watu akisema: “Atakayeujenga tena muji wa Yeriko, alaaniwe na Mungu. Yeyote atakayeweka musingi wa muji huo, muzaliwa wake wa kwanza akufe. Yeyote atakayejenga mulango wa muji huo, mwana wake kitenda mimba akufe.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 6:26
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati wa utawala wake, Hieli wa muji wa Beteli aliujenga upya muji wa Yeriko. Na sawa kabisa na neno Yawe alilosema kwa njia ya Yoshua mwana wa Nuni, Hieli alikufiwa na muzaliwa wake wa kwanza aliyeitwa Abiramu, wakati wa kuiweka misingi ya Yeriko. Akakufiwa vilevile na mwana wake mudogo aliyeitwa Segubu, wakati wa kuweka milango ya muji wa Yeriko.


Lakini mufalme akamwambia: “Nitakuapisha mara ngapi kwamba unaposema nami kwa jina la Yawe, unapaswa kuniambia ukweli mutupu?”


Kisha Elia akamwambia Elisha: “Tafazali ubakie hapa. Yawe amenituma niende Yeriko.” Lakini Elisha akakataa akisema: “Kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, sitakuacha.” Basi, wakaenda pamoja mpaka Yeriko.


Waedomu, wale wazao wa Esau, wanasema kwamba ingawa miji yao imeharibiwa, watajenga upya mabomoko yake. Lakini, Yawe wa majeshi anasema hivi: Wanaweza kuijenga upya, lakini mimi nitaibomoa tena. Watu watawaita: Taifa ovu ambalo Yawe amelikasirikia milele.


Lakini Yesu akanyamaza. Kuhani Mukubwa akamwambia: “Ninakuapisha kwa jina la Mungu Mwenye Uzima, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.”


Na kulikuwa Wayuda wamoja waliotangatanga huku na huko kwa kufukuza pepo. Watu wale wakajaribu vilevile kutaja jina la Bwana Yesu, wakiwaambia vilevile pepo: “Ninawaamuru muondoke kwa jina la Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo.”


Kutoka Yanoa ulikwenda hata Ataroti na Nara, hata kufika Yeriko, ambako uliishia katika muto Yordani.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ