Hivyo, hao wazao wakakuja na kurizi inchi. Ulishinda Wakanana na kuwatia katika mikono yao. Watu wako waliweza kuwatendea vile walivyotaka wafalme na watu wa inchi hiyo.
Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.
Milango ya kuingilia katika muji wa Yeriko ilikuwa imefungwa imara kwa ndani kwa kuwazuia Waisraeli wasiingie. Hakuna mutu aliyeweza kuingia wala kutoka katika muji huo.
Yawe akamwambia Yoshua: “Usiogope, wala usikuwe na wasiwasi wowote; uwatwae waaskari wako wote uelekee muji wa Ai, maana nimetia mufalme wa Ai katika mikono yako, pamoja na watu wake, muji wake na inchi yake.
Naye Yawe, Mungu wa Israeli, akamutia Sihoni pamoja na watu wake katika mikono ya Waisraeli, wakawashinda. Hivyo Waisraeli wakatwaa inchi yote ya Waamori ambao walikuwa wanaishi kule.
Tosheka na kile ambacho mungu wako Kemosi amekupa. Lakini inchi yoyote ambayo Yawe, Mungu wetu, amewafukuza wakaaji wake, akatupa sisi, hiyo ni mali yetu sisi.