Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 6:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Lakini feza yote, zahabu, vyombo vya shaba na chuma ni vitakatifu kwa Yawe; hivyo vitawekwa katika hazina ya Yawe.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 6:19
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa ajili ya Yawe, Daudi akatakasa zawadi zile, pamoja na feza na zahabu ambazo alikuwa ameziteka kwa mataifa yote aliyoyashinda,


Akaitwaa hazina yote ya nyumba ya Yawe na ya nyumba ya kifalme. Alitwaa kila kitu; naye alitwaa ngao zote za zahabu Solomono alizozitengeneza.


Basi, mufalme Solomono akamaliza kazi zote zilizoelekea nyumba ya Yawe. Kisha Solomono akaleta mali yote ambayo baba yake Daudi, alikuwa ameitoa kwa Bwana, ni kusema: feza, zahabu na vyombo; akaiweka katika hazina za nyumba ya Yawe.


Tena kama vile Yawe alivyosema, Nebukadneza alitwaa mali yote iliyokuwa ndani ya nyumba ya Yawe, na ndani ya nyumba ya kifalme. Akakatakata vyombo vyote vya zahabu ambavyo Solomono mufalme wa Israeli alitengeneza. Vyombo hivyo vilikuwa ndani ya hekalu la Yawe.


Zawadi zile, mufalme Daudi alizitakasa kwa ajili ya Yawe pamoja na feza na zahabu aliyonyanganya kwa mataifa yote, kutoka kwa: Waedomu, Wamoabu, Waamoni, Wafilistini na Waamaleki.


Kati ya Walawi, Ahia alielekea uangalizi wa hazina ya nyumba ya Mungu, na hazina na vitu vitakatifu.


Selomoti na wandugu zake, ndio waliokuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vitakatifu ambavyo mufalme Daudi alitoa kwa Mungu, viongozi wa jamaa, majemadari wa maelfu na mamia na majemadari wa jeshi.


Walichunga sehemu ya vitu walivyonyanganya katika vita kwa ajili ya kutengeneza nyumba ya Yawe.


Vilevile vitu vyote vilivyotolewa kwa Mungu na nabii Samweli na Saulo mwana wa Kisi, na Abeneri, na Yoabu mwana wa Zeruya, vilikuwa chini ya uangalizi wa Selomiti na wandugu zake.


Alimupatia mufano wa yote aliyokusudia ndani ya moyo juu ya viwanja vya nyumba ya Yawe, vyumba vya Mungu na gala za kuwekea vitu vitakatifu.


Alivirudisha katika nyumba ya Mungu vifaa vyote vilivyotakaswa na baba yake pamoja na vile alivyotakasa yeye mwenyewe; feza na zahabu na vyombo vingine.


na mule ndani wakaweka matoleo, sehemu moja za kumi na vyote vilivyotakaswa kwa uaminifu. Wakamuweka Konania, Mulawi, kuwa musimamizi mukubwa muchungaji wa vitu hivyo, na ndugu yake, Simea kuwa musaidizi wake.


Kila unga wetu wa kwanza, matoleo yetu, matunda ya miti, divai na mafuta tutavileta kwa kuhani kwenye vyumba vya nyumba ya Mungu wetu. Tena tutaleta zaka zetu za mazao yetu kwa Walawi, maana ndio wanaoshugulika na kukusanya zaka zile katika vijiji vyetu.


Basi, Ebedimeleki akatwaa watu hao na kwenda pamoja nao katika nyumba ya kifalme, wakaingia katika gala ya nyumba ya kifalme; Ebedimeleki akatwaa nguo zilizopasukapasuka na kuchakaa, akaziteremushia Yeremia ndani ya kisima kwa kamba.


Katika mwaka wa ine matunda yake yote yatakuwa matakatifu, yatatolewa kuwa sadaka ya sifa, kwa Yawe.


Yawe anasema: Enyi watu wa Sayuni, musimame muwakanyagekanyage! Nitawapatia nguvu kama ngombe dume mwenye pembe za chuma na kwato za shaba. Mutawasaga watu wa mataifa mengi; mutanitolea mimi mapato yao, mutanitolea mali zao mimi Bwana wa dunia yote.


Wakabeba vitu vyote walivyonyanganya na vile vyote walivyoteka na watu na ya nyama,


wakamupelekea Musa na Eleazari, na Waisraeli wote waliokuwa katika kambi katika inchi za mabonde za Moabu, ngambo ya Yordani karibu na Yeriko.


Zahabu, feza, shaba, chuma, manjanja na madini ya risasi,


Wakubwa wa makuhani wakaokota zile feza na kusema: “Kufuatana na Sheria yetu hairuhusiwi kuweka feza kama hizi ndani ya sanduku ya hekalu kwa sababu feza hizi ni za damu.”


Yesu akaikaa akielekea kwenye sanduku ya kutilia sadaka za hekalu. Akaangalia jinsi watu walivyotia feza ndani ya sanduku ile. Watajiri wengi walitia feza nyingi ndani yake.


Waisraeli wametenda zambi, maana wamelivunja agano langu nililowaamuru washike. Wametwaa vimoja kati ya vitu vilivyotolewa viangamizwe. Wameviiba na kudanganya, wakaviweka pamoja na vitu vyao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ